HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, March 29, 2018

MKUTANO MKUU WA YANGA SASA RASMI MEI 5

Na Zainab Nyamka,Globu ua Jamii

KATIBU Mkuu wa Klabu ya Yanga Charles Boniface Mkwasa ametangaza siku maalumu ambayo klabu itafanya mkutano mkuu wa wanachama wote,kujadili masuala mbalimbali muhimu ya maendeleo ambayo itakuwa Mei 5 mwaka huu.

Mkwasa amesema  kuwa wanachama wa Yanga wanapaswa kufanya maandalizi ya kuhudhuria mkutano huo sasa kwa kulipa ada zao mapema kwa sababu kwenye mkutano huo ukaguzi mkubwa utafanyika kabla ya watu kuingia ndani ya ukumbi.

Akizungumza leo ,Mkwasa amesema mkutano huo utafanyika Mei 5 mwaka huu jijini Dar es Salaam, hivyo wanachama wenye kadi aina zote mbili wataruhusiwa kuingia ukumbuni, kwa maana ya wale wote wenye kadi za zamani na kadi mpya zinazotolewa na benki ya Posta.

Akiendelea zaidi Mkwasa amesema  kupitia kikao cha kamati ya utendaji kilichofanyika Jumapili iliyopita, kamati   imeridhia kufanyika kwa Mkutano huo, na kuomba wanachama kujindaa kwa ajenda ambazo zitatangazwa baaadae.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad