MALKIA wa muziki wa Bongo fleva nchini, Judith Wambura a.k.a Lady Jaydee ametaja majina ya wasanii wengine watakaomsindikiza katika Tamasha la Unaweza linalotarajia kufanyika Machi 31 mwaka katika Hotel ya Golden Tulip Ostetbay.
Akizungumza na Michuzi blog Jaydee amewataja wasanii hao ni Bushoke, Nick Mbishi, Alawi Junior na Wengine wengi.
"Hii ni shoo ambayo nataka kila mtu afurahie muziki akiwa nyumbani na ladha ambazo walikuwa wamezikosa kwa muda mrefu, hivyo kupitia onesho hilo nitaka kiu yao ya kutonusikia kwa muda kidogo," amesema Jaydee
Aidha mwanamuziki huyo amesema siku hiyo kutakuwa na watu maarufu akiwamo MC Pilipili na wengine wengi.
Amesema maandalizi ya shoo hiyo yamekamilika na kwamba amejiandaa vya kutosha.
Amefafanua shoo hiyo itaanza saa12 jioni ambapo Machozi Band watakuwa jukwaani na kumalizika saa sita usiku atamaliza lakini ana uhakika watakaofika watakuwa wameandika historia ya aina yake kutokana na namna alivyojiandaa.
No comments:
Post a Comment