Na John Nditi, Morogoro
UONGOZI wa Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM) kinatarajia kujenga kampasi tawi la Kigamboni, Jijini Dar es Salaam itakayo kutoa shahada mbalimbali za masomo ya usimamizi wa biashara na kwa kuanzia na udahili wa wanafunzi 5,000.
Chuo hicho Kampasi ya Kigamboni ni kuwezesha kupata wataalamu wengi wa usimamizi wa biashara watakaokidhi mahitaji ya soko la ajira katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).
Makamu mkuu wa Chuo Kikuu hicho, Profesa Hamza Njozi,alisema wakati wa uwekeji wa jiwe la msingi kitakapojengwa eneo la Lingato , Kata ya Kisarawe II ,Manispaa ya Kigamboni , Jijini Dar es Salaam.
Profesa Njozi alisema, tangu kuanzishwa kwa Chuo hicho Oktoba 23, 2004 chini ya Mfuko wa Taasisi ya Maendeleo ya Waislamu (MDF) na kilizinduliwa rasmi Oktoba 22, 2005 na Rais wa Serikali ya awamu ya tatu , Benjamin William Mkapa .
Makamu Mkuu wa Chuo hicho alisema, hadi kufikia mahafali ya kumi mwaka jana ,kimeshatoa wahitimu 5,433 wa ngazi ya Shahada, Stashahada na Astashahada ambapo kwa sasa kina zaidi ya wanafunzi 3,000 na uwezo wa chuo ni kuchukua wanafunzi 8,000.
Profesa Njozi alisema , kujengwa kampasi Tawi la Kigamboni kunatarajiwa kuongeza udahili wa wanafunzi wa ndani na n je ya nchi baada ya uongozi wa Chuo kupata eneo la ardhi lenye ukubwa wa ekari 400 kwa ajili ya ujenzi huo.
Makamu Mkuu wa Chuo hicho alisema ,kitakapo kamilika kitakuwa cha kimataifa na mahitaji yote muhimu yatakayomwezesha mwanafunzi kusoma kwa ufanisi.
“ ….Hiki chuo kitakuwa ni cha kipekee , tutatumia wahadhiri kutoka nchi mbalimbali Duniani kufundisha kwa njia ya Moduli , tunataka mwanafunzi akitoka hapa awe amekamilika kuingia kwenye soko la ajira za ushindani wa kimataifa “ alisema Profesa Njozi.
Hata hivyo alisema ,hati miliki ya kisheria ya eneo hilo wanazo ikiwemo pia michoro ya namna ya chuo kitakavyokuwa imekamilika ikijumisha majengo ya kisasa ya utawala, taaluma , madarasa pamoja na ya chakula.
Alisema ,makadirio ya haraka ya ujenzi huo unataria kugharimu zaidi ya Sh bilioni 47 hadi kukamilika kwake na muda muafaka utakapowadia ujenzi wa Chuo Kampasi ya Kigamboni utaanza.
“ Tupo mbioni kumpata mkandarasi kwa ajili ya kukamilisha taratibu za maandalizi ya awali kabla ya kuanza ujenzi wa chuo hiki” alisema Profesa Njozi.
Profesa Njozi , alisema licha ya Chuo Kikuu hicho bado ni kichanga , jina lake linaendelea kustawi na kuchanua , ambapo Watanzania wengi wamekiamini kutokana na ubora wa taaluma na malezi yanayotolewa Chuoni hapo.
Alisema ,kwa sasa Chuo Kikuu kinatoa elimu ya kumwezesha pia mhitimu kumudu kufanya kazi mahali popote pale ikiwemo za kujitengemea badala ya kusubiri kazi za kuajiriwa ambazo ni chache.
Naye Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo cha MUM (MUMSO) , Yahya Khamis alisema Chuo hicho kinatekeleza sera ya Serikali ya awamu ya tano ya Rais , Dk John Magufuli inayohimiza Tanzania ya Viwanda.
Alisema kuwa, ujenzi wa Chuo hicho ni fursa nzuri ya kuchochjea utekelezaji wake kwa kuwapata wataalamu wa usimamizi wa biashara viwandani.
“ Naiomba Serikali iongeze nguvu ili kufanikisha ujenzi huu kwa kuwa wasomi wanaotoka hapa watakwenda kusaidia katika azma ya kuifanya Tanzania ya Viwanda “ alisema Khamis.
Makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM) , Profesa Hamza Njozi akipanda mti baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Kampasi yake itakayo kutoa shahada mbalimbali za masomo ya usimamizi wa biashara itakayojengwa eneo la Lingato , Kata ya Kisarawe II, Manispaa ya Kigamboni, jijini Dar es Salaam.
Makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM) , Profesa Hamza Njozi ( wapili kushoto fulana pundamilia) akibadirishana mawazo na mmoja wa viongozi wa Chuo hicho baada ya uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa Kampasi ya Kigamboni itakayo kutoa shahada mbalimbali za masomo ya usimamizi wa biashara itakayojengwa eneo la Lingato , Kata ya Kisarawe II ,Manispaa ya Kigamboni, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi wakiume wa Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM) wakisaidia kubeba tofari hadi eneo la uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Kampasi ya Kigamboni itakayo kutoa shahada mbalimbali za masomo ya usimamizi wa biashara itakayojengwa eneo la Lingato , Kata ya Kisarawe II ,Manispaa ya Kigamboni, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wanafunzi wakike wa Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM) wakisaidia kusogeza mfuko wa saruji kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Kampasi yake itakayo kutoa shahada mbalimbali za masomo ya usimamizi wa biashara itakayojengwa eneo la Lingato , Kata ya Kisarawe II ,Manispaa ya Kigamboni, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi na watumishi wa Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM) wakisaidiana kuchimba msingi wa uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Kampasi ya Kigamboni itakayo kutoa shahada mbalimbali za masomo ya usimamizi wa biashara itakayojengwa eneo la Lingato , Kata ya Kisarawe II ,Manispaa ya Kigamboni, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wanafunzi wakike wa Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Kampasi yake itakayo kutoa shahada mbalimbali za masomo ya usimamizi wa biashara itakayojengwa eneo la Lingato , Kata ya Kisarawe II ,Manispaa ya Kigamboni, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi na watumishi wengine wa Chuo cha Waislamu cha Morogoro (MUM) wakiwa kwenye eneo itakapojengwa Kampasi ya Kigamboni ya Chuo kikuu hicho.
( Picha na John Nditi).
No comments:
Post a Comment