HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, February 15, 2018

SIMIYU YAJIPANGA KIMKAKATI KUONGEZA KIWANGO CHA UFAULU KWENYE ELIMU

Na Stella Kalinga, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu
Mkoa wa Simiyu umejipanga kimkakati katika  kuhakikisha unaongeza ufaulu kwenye Elimu na kuwa miongoni mwa mikoa inayofanya vizuri Kitaifa kutoka mahali ulipo sasa,  kwenda kwenye nafasi ya tarakimu moja(single digit) yaani nafasi ya kwanza hadi ya tisa.

Hayo yalibainishwa katika kikao maalum kilichofanyika jana Mjini Bariadi kati ya Viongozi na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na baadhi ya walimu (mahiri) ambao walifanya vizuri katika masomo yako kwenye Matokeo ya mitihani ya Kitaifa mwaka 2017, kilichofanyika jana Mjini Bariadi.

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini amewataka walimu pamoja na watendaji wengine wa idara ya Elimu kuongeza bidii katika maeneo yao ili waweze kuufikisha mkoa katika nafasi ya tarakimu moja (single digit) kwa kuwa sababu, uwezo na nia ya kufika hapo ipo.

“Watu wa Sekta ya elimu Ombi langu kwenu wakati tukiwa tunajipongeza kuwa wa 14 katika mtihani wa kidato cha nne mwaka 2017 tudhamirie kuongeza bidii ili tuingia kwenye ‘single digit’, sababu za kuingia kwenye ‘single digit’ zipo, uwezo upo kwa kuwa ninyi mpo na nia ya Simiyu kuonekana juu tunayo” alisema Sagini.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema  miongoni mwa mambo yatakayofanya mkoa huo kuendelea kufanya vizuri ni pamoja na kuendeleza makambi kwa wanafunzi wa madarasa ya mitihani ambayo yatasaidia kuwaandaa vema na Mitihani ya Taifa.

Aidha, Mtaka amesema mkoa huo umeandaa Mpango Mkakati wa TEHAMA ambayo katika sekta ya elimu itasaidia kutekeleza mpango wa madarasa ya mitihani kusoma kwa kupitia mitandao na tayari umepokea kompyuta 60 kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi  ambazo zitaweka katika shule zenye mifumo ya TEHAMA ili kuwezesha mpango huo.

Wakati huo huo Mtaka amesisitiza juu ya eneo la umuhimu wa chakula kwa wanafunzi ambapo amemuagiza Afisa Elimu Mkoa kuitisha kikao cha Wenyeviti wa Kamati za Shule, waweze kuzungumza namna ya nzuri ya kuwawezesha wanafunzi kula chakula wawapo shuleni, ili wasome vizuri baadaye waweze kufanya vizuri katika masomo yao..

“ Kama tunataka kuwa mkoa bora na kushindana kwenye elimu wazazi wakubali kuchangia chakula ili watoto wale shuleni, nitakaa na wazazi niwaambie ukweli watoe sehemu ya chakula cha nyumbani kije shuleni  na waweke utaratibu wa kuwapikia watoto ili wale shuleni; mtoto akiona moshi jikoni akili inachemka” alisema Mtaka.

Kwa upande wake Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu, Mwl.Julius Nestory alisema uwezo wa mkoa huo  kufikia nafasi ya tarakimu moja(single digit) upo  kwa kuwa,  tangu mkoa huo ulipoanzishwa mwaka 2012 umekuwa ukifanya vizuri hususani katika Mtihani wa Kidato cha Nne, ambapo ulitoka katika nafasi ya 17, nafasi ya  14 miaka miwili mfululizo na kufikia nafasi ya 11 mwaka 2017.

Nao baadhi ya walimu wakuu na wakuu wa shule walisema ili kufikia azma ya Mkoa huo kushika nafasi ya tarakimu moja yaani nafasi ya kwanza hadi ya tisa(single digit) wamejipanga katika kusimamia mipango mkakati ya shule zao, kuendeleza mazoezi ya mara kwa mara, kuongeza ushirikiano na wazazi, kufautilia ratiba na kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia.

“Kilichonisaidia mpaka shule yangu ikawa ya pili kimkoa katika mtihani wa darasa la nne ni ushirikiano na wazazi, mitihani ya ujirani mwema, watoto kula chakula cha mchana shuleni pamoja na kuhakikisha walimu wanafuata ratiba ya masomo” alisema Joseph Kasoka Mwalimu Mkuu Shule ya msingi Halawa  wilayani Bariadi.

Kikao cha watendaji wa Idara ya Elimu kiliwahusisha Maafisa Elimu wa Wilaya, Wadhiti Ubora wa Elimu, Waratibu wa Elimu Kata, Wakuu wa Shule, Walimu Wakuu na baadhi ya Walimu waliofanya vizuri katika masomo yao kwenye  Mitihani ya Kitaifa mwaka 2017, lengo likiwa nikutambua juhudi zilizofanyika kwa mwaka 2017.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka akizungumza na Viongozi na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na baadhi ya walimu (mahiri) ambao walifanya vizuri katika masomo yako kwenye Matokeo ya mitihani ya Kitaifa mwaka 2017, katika kikao kilichofanyika jana Mjini Bariadi.
 Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini akizungumza na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na baadhi ya walimu (mahiri) ambao walifanya vizuri katika masomo yako kwenye Matokeo ya mitihani ya Kitaifa mwaka 2017, katika kikao kilichofanyika jana Mjini Bariadi.
 Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl.Julius Nestory akizungumza na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na baadhi ya walimu (mahiri) ambao walifanya vizuri katika masomo yako kwenye Matokeo ya mitihani ya Kitaifa mwaka 2017, katika kikao kilichofanyika jana Mjini Bariadi..
 Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwasubuya iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi ambayo ilikuwa ya kwanza Kimkoa katika Mtihani wa Darasa la Nne 2017 akieleza uzoefu wake mbele ya walimu wenzake na viongozi wa idara ya elimu, katika kikao kilichofanyika jana Mjini Bariadi.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Ndg.Abdallah Malela akizungumza na Viongozi na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na baadhi ya walimu (mahiri) ambao walifanya vizuri katika masomo yako kwenye Matokeo ya mitihani ya Kitaifa mwaka 2017, katika kikao kilichofanyika jana Mjini Bariadi.
 Mwalimu Aron Kiunsi wa Shule ya Sekondari Bariadi akipokea Cheti kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka kama mwalimu mahiri wa somo la Kiingereza katika Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne mwaka 2017, katika kikao cha viongozi na watendaji wa Elimu kilichofanyika jana Mjini Bariadi.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka (wa tano kulia) akiwa katika picha ya pamoja na walimu mahiri kwenye masomo mbalimbali katika Mitihani ya Kitaifa mwaka 2017 mara baada ya kikao cha Viongozi na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na walimu hao, kumalizika jana mjini Bariadi.
 Baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na baadhi ya walimu (mahiri) ambao walifanya vizuri katika masomo yako kwenye Matokeo ya mitihani ya Kitaifa mwaka 2017, wakifuatilia masuala mbalimbali katika kikao kilichofanyika jana Mjini Bariadi.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini(wa nne kushoto mbele) akiwa katika picha ya pamoja na walimu mahiri kwenye masomo mbalimbali katika Mitihani ya Kitaifa mwaka 2017 mara baada ya kikao cha Viongozi na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na walimu hao, kumalizika jana mjini Bariadi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad