Na Stella Kalinga, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu
Mkoa
wa Simiyu umejipanga kimkakati katika kuhakikisha unaongeza ufaulu
kwenye Elimu na kuwa miongoni mwa mikoa inayofanya vizuri Kitaifa kutoka
mahali ulipo sasa, kwenda kwenye nafasi ya tarakimu moja(single digit)
yaani nafasi ya kwanza hadi ya tisa.
Hayo
yalibainishwa katika kikao maalum kilichofanyika jana Mjini Bariadi
kati ya Viongozi na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya,
Kata na baadhi ya walimu (mahiri) ambao walifanya vizuri katika masomo
yako kwenye Matokeo ya mitihani ya Kitaifa mwaka 2017, kilichofanyika
jana Mjini Bariadi.
Katibu
Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini amewataka walimu pamoja na
watendaji wengine wa idara ya Elimu kuongeza bidii katika maeneo yao ili
waweze kuufikisha mkoa katika nafasi ya tarakimu moja (single digit)
kwa kuwa sababu, uwezo na nia ya kufika hapo ipo.
“Watu
wa Sekta ya elimu Ombi langu kwenu wakati tukiwa tunajipongeza kuwa wa
14 katika mtihani wa kidato cha nne mwaka 2017 tudhamirie kuongeza bidii
ili tuingia kwenye ‘single digit’, sababu za kuingia kwenye ‘single
digit’ zipo, uwezo upo kwa kuwa ninyi mpo na nia ya Simiyu kuonekana juu
tunayo” alisema Sagini.
Naye
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema miongoni mwa mambo
yatakayofanya mkoa huo kuendelea kufanya vizuri ni pamoja na kuendeleza
makambi kwa wanafunzi wa madarasa ya mitihani ambayo yatasaidia
kuwaandaa vema na Mitihani ya Taifa.
Aidha,
Mtaka amesema mkoa huo umeandaa Mpango Mkakati wa TEHAMA ambayo katika
sekta ya elimu itasaidia kutekeleza mpango wa madarasa ya mitihani
kusoma kwa kupitia mitandao na tayari umepokea kompyuta 60 kutoka Tume
ya Taifa ya Sayansi ambazo zitaweka katika shule zenye mifumo ya TEHAMA
ili kuwezesha mpango huo.
Wakati
huo huo Mtaka amesisitiza juu ya eneo la umuhimu wa chakula kwa
wanafunzi ambapo amemuagiza Afisa Elimu Mkoa kuitisha kikao cha
Wenyeviti wa Kamati za Shule, waweze kuzungumza namna ya nzuri ya
kuwawezesha wanafunzi kula chakula wawapo shuleni, ili wasome vizuri
baadaye waweze kufanya vizuri katika masomo yao..
“
Kama tunataka kuwa mkoa bora na kushindana kwenye elimu wazazi wakubali
kuchangia chakula ili watoto wale shuleni, nitakaa na wazazi niwaambie
ukweli watoe sehemu ya chakula cha nyumbani kije shuleni na waweke
utaratibu wa kuwapikia watoto ili wale shuleni; mtoto akiona moshi
jikoni akili inachemka” alisema Mtaka.
Kwa
upande wake Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu, Mwl.Julius Nestory alisema
uwezo wa mkoa huo kufikia nafasi ya tarakimu moja(single digit) upo
kwa kuwa, tangu mkoa huo ulipoanzishwa mwaka 2012 umekuwa ukifanya
vizuri hususani katika Mtihani wa Kidato cha Nne, ambapo ulitoka katika
nafasi ya 17, nafasi ya 14 miaka miwili mfululizo na kufikia nafasi ya
11 mwaka 2017.
Nao
baadhi ya walimu wakuu na wakuu wa shule walisema ili kufikia azma ya
Mkoa huo kushika nafasi ya tarakimu moja yaani nafasi ya kwanza hadi ya
tisa(single digit) wamejipanga katika kusimamia mipango mkakati ya shule
zao, kuendeleza mazoezi ya mara kwa mara, kuongeza ushirikiano na
wazazi, kufautilia ratiba na kuboresha mazingira ya kujifunzia na
kufundishia.
“Kilichonisaidia
mpaka shule yangu ikawa ya pili kimkoa katika mtihani wa darasa la nne
ni ushirikiano na wazazi, mitihani ya ujirani mwema, watoto kula chakula
cha mchana shuleni pamoja na kuhakikisha walimu wanafuata ratiba ya
masomo” alisema Joseph Kasoka Mwalimu Mkuu Shule ya msingi Halawa
wilayani Bariadi.
Kikao
cha watendaji wa Idara ya Elimu kiliwahusisha Maafisa Elimu wa Wilaya,
Wadhiti Ubora wa Elimu, Waratibu wa Elimu Kata, Wakuu wa Shule, Walimu
Wakuu na baadhi ya Walimu waliofanya vizuri katika masomo yao kwenye
Mitihani ya Kitaifa mwaka 2017, lengo likiwa nikutambua juhudi
zilizofanyika kwa mwaka 2017.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka akizungumza na Viongozi na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na baadhi ya walimu (mahiri) ambao walifanya vizuri katika masomo yako kwenye Matokeo ya mitihani ya Kitaifa mwaka 2017, katika kikao kilichofanyika jana Mjini Bariadi.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini akizungumza na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na baadhi ya walimu (mahiri) ambao walifanya vizuri katika masomo yako kwenye Matokeo ya mitihani ya Kitaifa mwaka 2017, katika kikao kilichofanyika jana Mjini Bariadi.
Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl.Julius Nestory akizungumza na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na baadhi ya walimu (mahiri) ambao walifanya vizuri katika masomo yako kwenye Matokeo ya mitihani ya Kitaifa mwaka 2017, katika kikao kilichofanyika jana Mjini Bariadi..
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwasubuya iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi ambayo ilikuwa ya kwanza Kimkoa katika Mtihani wa Darasa la Nne 2017 akieleza uzoefu wake mbele ya walimu wenzake na viongozi wa idara ya elimu, katika kikao kilichofanyika jana Mjini Bariadi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Ndg.Abdallah Malela akizungumza na Viongozi na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na baadhi ya walimu (mahiri) ambao walifanya vizuri katika masomo yako kwenye Matokeo ya mitihani ya Kitaifa mwaka 2017, katika kikao kilichofanyika jana Mjini Bariadi.
Mwalimu Aron Kiunsi wa Shule ya Sekondari Bariadi akipokea Cheti kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka kama mwalimu mahiri wa somo la Kiingereza katika Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne mwaka 2017, katika kikao cha viongozi na watendaji wa Elimu kilichofanyika jana Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka (wa tano kulia) akiwa katika picha ya pamoja na walimu mahiri kwenye masomo mbalimbali katika Mitihani ya Kitaifa mwaka 2017 mara baada ya kikao cha Viongozi na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na walimu hao, kumalizika jana mjini Bariadi.
Baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na baadhi ya walimu (mahiri) ambao walifanya vizuri katika masomo yako kwenye Matokeo ya mitihani ya Kitaifa mwaka 2017, wakifuatilia masuala mbalimbali katika kikao kilichofanyika jana Mjini Bariadi.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini(wa nne kushoto mbele) akiwa katika picha ya pamoja na walimu mahiri kwenye masomo mbalimbali katika Mitihani ya Kitaifa mwaka 2017 mara baada ya kikao cha Viongozi na Watendaji wa Idara ya Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na walimu hao, kumalizika jana mjini Bariadi.
No comments:
Post a Comment