HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, February 14, 2018

Rais Magufuli amteua Meja Jenerali Yakubu Hassan kuwa Mnadhimu Mkuu wa JWTZ

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 14 Februari, 2018 amemteua Meja Jenerali Yakubu Hassan Mohamed kuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Pamoja na uteuzi huo, Mhe. Rais Magufuli amempandisha cheo kutoka Meja Jenerali na kuwa Luteni Jenerali.

Luteni Jenerali Yakubu Hassan Mohamed anachukua nafasi ya Luteni Jenerali James Alois Mwakibolwa ambaye amestaafu.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewapandisha vyeo kutoka Brigedia Jenerali na kuwa Meja Jenerali wafuatao;
  1.     Brig Jen. J.G. Kingu
  2.     Brig Jen. M.S. Busungu
  3.     Brig Jen. R.R. Mrangira
  4.     Brig Jen. B.K. Masanja
  5.     Brig Jen. G.T. Msongole
  6.     Brig Jen. A.F. Kapinga
  7.     Brig Jen. K.P. Njelekela
  8.     Brig Jen. A.S. Bahati
  9.     Brig Jen. M.E. Mkingule
  10.     Brig Jen. S.S. Makona
Mabrigedia Jenerali wote waliopandishwa vyeo watapangiwa vituo vya kazi baadaye.

Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Yakubu Hassan Mohamed ataapishwa kesho tarehe 15 Februari, 2018 saa 5:00 asubuhi Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
14 Februari, 2018

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad