HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, February 19, 2018

MASAUNI AFUNGUA KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

 Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza wakati akifungua Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani  ya  Nchi. Lengo la baraza hilo ni kujadili utendaji na maendeleo ya kila idara katika kutimiza majukumu ya wizara. Kikao hicho kimefanyika  katika Ukumbi wa Maafisa Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,  Mhandisi Hamad  Masauni (watatu kulia), na  Naibu Katibu Balozi Hassan Simba Yahya (wanne kulia), wakiimba wimbo wa mshikamano wakati wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo kilichofanyika katika Ukumbi wa Maafisa Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. Lengo la baraza hilo ni kujadili utendaji na maendeleo ya kila idara katika kutimiza majukumu ya wizara .Wengine ni  viongozi wa Chama cha Wafanyakazi  tawi la wizara hiyo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,Thobias Andengenye, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk. Anna Makakala na Kamishna   wa Magereza anayeshughulikia  Utawala na Fedha, Gaston Sanga wakiimba  wimbo wa mshikamano wakati wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, lengo la baraza hilo ni kujadili utendaji na maendeleo ya kila idara katika kutimiza majukumu ya wizara.Kikao hicho kimechofanyika katika Ukumbi wa Maafisa Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma kwa Jamii, Aloyce Musika,  akiongoza Wakuu wengine wa vitengo vya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kuimba wimbo wa mshikamano wakati wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo kilichofanyika katika Ukumbi wa Maafisa Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,Thobias Andengenye,akichangia hoja wakati wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Lengo la baraza hilo ni kujadili utendaji na maendeleo ya kila idara katika kutimiza majukumu ya wizara.Kikao hicho kimechofanyika katika Ukumbi wa Maafisa Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam leo.Wengine ni Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk. Anna Makakala na Kamishna   wa Magereza anayeshughulikia  Utawala na Fedha, Gaston Sanga. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk. Anna Makakala, akichangia hoja wakati wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Lengo la baraza hilo ni kujadili utendaji na maendeleo ya kila idara katika kutimiza majukumu ya wizara.Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Maafisa Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam leo.Wengine ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,Thobias Andengenye(kushoto) na Kamishna wa Magereza anayeshughulikia  Utawala na Fedha, Gaston Sanga. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Kamishna wa Magereza anayeshughulikia  Utawala na Fedha, Gaston Sanga, akichangia hoja wakati wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Lengo la baraza hilo ni kujadili utendaji na maendeleo ya kila idara katika kutimiza majukumu ya wizara.Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Maafisa Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam leo.Wengine ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye (kushoto) na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk. Anna Makakala. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu, akichangia hoja wakati wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Maafisa Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad