HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, January 8, 2018

UCHAGUZI MDOGO JIMBO LA SONGEA MJINI WAZIDI KUIMALIZA KAMBI YA UPINZANI

Moses Machali akimnadi Dkt Damas Ndumbaro
Na Nathan Mtega, Jamvi la habari - Songea

Wakati kampeni za kuelekea uchaguzi mdogo wa jimbo la Songea mjini mkoani Ruvuma zikiendelea katika kata mbalimbali za manisipaa ya Songea mkoani Ruvuma kwa ajili ya kumpata mbunge wa jimbo hilo ambaye chama cha mapinduzi kimemteua Dkt Damas Ndumbaro kupeperusha bendera ya chama hicho waliokuwa viongozi na wanachama wa vyama vya upinzani nchini wamezidi kujitokeza kwenye kampeni hizo na kutangaza kuachana na vyama vyao vya awali.

Miongoni mwa viongozi hao wa vyama vya upinzani ni pamoja na waliokuwa wajumbe watatu wa serikali ya mtaa wa Majengo mjini Songea kwa tiketi ya chama cha demokrasia na maendeleo ambao walitangaza uamuzi huo wa kukihama chao hicho na kujiunga na chama cha Mapinduzi baada ya hotuba ya siku mbili mfululizo kwenye kampeni hizo za kumnadi mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya chama cha mapinduzi iliyotolewa na aliyewahi kuwa mwanachama wa chama na kingozi pia cha Demokrasia na maendeleo Moses Machali.

Katika hotuba yake ya kumnhadi mgombea huyo Machali alieleza sifa alizo nazo mgombea Dkt Damas Ndumbaro ambazo alizifahamu muda mrefu tangu akiwa kwenye kambi ya upinzani ambazo alisema hazina mashaka yoyote ya kumfanya asichaguliwe kuwa mwakilishi wa wananchi wa jimbo hilo na kuwataka wananchi wa jimbo la Songea mjini kwa ujumla kuitokeza kwa wingi siku ya Januari 13 mwaka huu kumpigia kura mgombea huyo na kuacha kuendelea kusikiliza na kufuata propaganda za wagombea wa vyama vya upinzani ambao walio wengi hawajui kilichoko kwenye vyama hivyo vya upinzani kwa sababu yeye alikuwepo huko na anajua kulivyo.

Viongozi wengine wa kambi ya upinzani waliopanda jukwaani katika viwanja vya mikutano vya Majengo na kutangaza kujiunga na chama cha mapinduzi ni pamoja na aliyekuwa katibu wa chama cha ACT Wazalendo mkoa wa Kigoma Sharon Msanya ambaye kabla ya kutangaza kujiunga na chama cha mapinduzi aliwataka wapiga kura wa jimbno la Songea mjini kutokuthubutu kulifanya jimbo hilo kuwa kambiya upinzani kwa sababu kufanya ni kurudisha nyuma jitihada za serikali za kuwaletea wananchi maendeleo ambayo wameyahityaji kwa muda mrefu kurtoka serikalini na serikali ya awamu ya tano inaendelea kuonesha dhamira ya dhati kuwafikishia wananchi maendeleo hayo.

Alisema yeye amekuwa kiongozi mkubwa wa chama cha ACT Wazalendo katika ngazi ya mkoa lwa Kigoma akini amefikia uamuzi huo wa kusafiri kutoka mkoani Kigoma mpaka mjini Songea ili aweze kupata fursa ya kuwaeleza wananchi wa Songea umuhimu wa kukiunga mkono chama cha mapinduzi na mgombea wake Dkt Dams Ndumbaro kwa ajili ya maendeleo yao na taifa kwa ujumla kwa sababu mgombea huyo amekuwa mpigania maendeleo ya taifa kwa muda mrefu hata kabla hajafikia uamuzi huo wa kugombea nafasi hiyo ya kuwawakilisha wananchi wa jimbo lake.

Huku naye Edna Sunga aliyekuwa katibu wa kamati ya maendeleo ya jamii taifa na mjumbe wa kamati kuu na halmashauri kuu taifa wa chama cha ACT Wazalendo akizungumza baada ya kukihama chama hico na kujijnga na chama cha mapinduzi amesema kwa sababu yeye ni muumini wa kuzingatia miiko na vita dhidi ya rushwa na kuwaletea maendeleo wananchi ameona hana sababu ya kuendelea kuwa kwenye upinzani badala ya kuongeza na kujnganisha nguvu ya kuwajhudumia wananchi walio wengi.

Amesema kiongozi au mwananchi yeyote mwenye dhamira ya dhati ya maendeleo ambayo wananchi walio wengi wanayahitajihana budi kukiunga mkopno chama cha mapinduzi na mgombea wake ambaye amevaa taswira ya chama hicho na taifa kwa ujumla huku naye mgombea wa jimbo hilo kwenye uchaguzi huo akiendelea kuwaomba wananchi wa mji wa Songea kujiktokeza kwa wingi siku hiyo ya uchaguzi kwa ajili ya kupiga kura kwa chama cha mapinduzi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad