HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, January 3, 2018

MAKAMU WA RAIS AHUDHURIA MSIBA WA MKE WA KANGI LUGOLA

​Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 3, Januari, 2018 amehani msiba wa Kamishna Msaidizi wa Polisi Mary Lugola ambaye ni Mke wa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. Kangi Lugola.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Kangi Lugola alipofika kutoa pole ya msiba wa mke wa Kangi Lugola, Kamishna Msaidizi wa Polisi Mary Lugola aliyefariki siku ya tarehe 01, Januari, 2018 katika hospitali ya Rabininsia jijini Dar es Salaam.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini kitabu cha maombolezo ya msiba wa mke wa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe.Kangi Lugola, Kamishna Msaidizi wa Polisi marehemu Mary Lugola aliyefariki siku ya tarehe 01, Januari, 2018 katika hospitali ya Rabininsia jijini Dar es Salaam.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiifariji familia ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe.Kangi Lugola wakati alipoenda kuwapa pole ya msiba wa Kamishna Msaidizi wa Polisi marehemu Mary Lugola nyumbani kwao klabu ya reli, Gerezani, jijini Dar es Salaam.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe.Kangi Lugola wakati alipoenda kutoa pole ya msiba wa mke wake Kamishna Msaidizi wa Polisi marehemu Mary Lugola aliyefariki siku ya tarehe 01, Januari, 2018 katika hospitali ya Rabininsia jijini Dar es Salaam.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapa pole watoto wa  marehemu Mary Lugola , mke wa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Kangi Lugola aliyefariki siku ya tarehe 01, Januari, 2018 katika hospitali ya Rabininsia jijini Dar es Salaam.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad