HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, January 18, 2018

DK. MAHIGA AHIMIZA MAZINGIRA MAZURI KUVUTIA WAWEKEZAJI

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Dk.Augustine Mahiga amesema kuwa ili kufikia uchumi wa viwanda ni muhimu kutengeneza mazingira mazuri ya kuwavutia wawekezaji katika sekta mbalimbali zikiwamo za sheria, kodi, ajira,vvivutio vya uwekezaji na kilimo.

Dk.Mahiga, ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati anazungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza kuzindua kongamano la siku mbili lililoandaliwa na Ubalozi wa India nchini Tanzania kwa kushirikisha nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) pamoja na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).

Lengo la kongamano hilo pamoja na mambo mengine washiriki wamezungumzia namna ya ushiriki wa sasa na siku zijazo unavyoweza kuleta amani katika nchi wanachama wa jumuiya hizo.Kauli mbiu ya kongamano katika kongamano hilo inasema "Amani, utulivu na maendeleo".

Dk. Mahiga amefafanua jambo hilo si jipya kuzungumzwa isipokuwa bado halijaeleweka na hivyo linatakiwa kuzunguzwa Tanzania pamoja EAC.

“Tunamkakati madhubuti wa kujenga viwanda katika EAC na SADC. Sasa kusema nataka viwanda ni kingine, kuvuta viwanda ni kingine, kufanya viwanda vizalishe na vistawi ni jambo lingine.

"Na ukisema unataka viwanda mazingira yapo?  unataka kufanikisha viwanda je  utaalam upo? hapo sasa kupitia mambo hayo matatu unaweza kuendesha viwanda,” amesema Dk.Mahiga.

Ameongeza katika kongamano hilo watazungumzia kinadharia kuhusu amani na jumuiaya hizo zinavyochagia kuleta amani katika nchi na namna mchanganyiko wa amani unavyoweza kuleta maendeleo katika mataifa hayo yanayoshirikiana.

Amewakumbusha washiriki wa kongamano hilo kuwa "Hapa tumekumbuka mchango wa mwanaharakati mkubwa Mahatma Ghandhi aliyeliyesisimua dunia kutokana na mapambano yake na Waingereza ili kuleta uhuru wa wa India na viongozi wengi wa Afrika waliiga mfano huo na hata Hayati Mwalimu Jualias Nyerere aliwahi kusema kuwa alijifunza kutoka kwake.

Pia Dk. Mahiga amesema nchi ya India ni kubwa na ina watu zaidi ya Sh.bilioni 1.2 na wana amani na wamekuwa wakifanya uchaguzi kwa demokrasia na kubwa zaidi wamejiimarisha kiuchumi na kuwa miongoni mwa nchi ambazo uchumi wake upo imara na kueleza ipo haja kwa nchi nyingine kuiga kutoka Taifa hilo.

"Amani inaweza kutazamiwa ndani ya nchi kama unatengeneza taasisi za  ushirikishi na uwajibikaji na si tu kudumisha amani bali kuleta utulivu wa kisiasa,"amesema Dk.Mahiga.

Naye aliyewahi kuwa Balozi wa Kwanza nchini India mwaka 1994 na Waziri Mkuu Mstaafu, Dk. Salim Ahmed Salim, amesifu uhusiano wa kidiplomasia uliopo kati ya Tanzania na India na hayo ni matunda ya Hayati Mwalimu Nyerere na Waziri Mkuu wa kwanza wa India  Jawaharial Nehru.

Kwa upande wa Balozi wa India nchini, Sandeep Arya, amesema pamoja na kujadili masuala ya ushirikiano Serikali ya India itatumia fursa ya kongamano hilo kukusanya maoni, mapendekezo na taarifa ambayo yatatolewa na washiriki waliopo na pamoja na wadau hasa wamasuala ya ulinzi, amani na maendeleo ili kila Taifa lifikie malengo ya kitaifa na kuboresha maisha ya wananchi wake.

Ameelezea namna ambavyo India imekuwa ikishirikiana na nchi zilizopo Bara la Afrika ikiwamo Tanzania katika kufanikisha upatikanaji wa maendeleo kwenye nyanja mbalimbali.
 Waziri Mkuu Mstaafu, Dk. Salim Ahmed Salim akizungumza leo jijini Dar es Salaam kwenye Kongamano la siku mbili lililoandaliwa na Ubalozi wa India nchini Tanzania kwa kushirikisha nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) pamoja na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Dk.Augustine Mahiga akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati akifungua rasmi Kongamano la siku mbili ambalo limeandaliwa na Ubalozi wa India nchini Tanzania.Kauli mbiu ya kongamano hilo ni Amani, Utulivu na Maendeleo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad