HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, December 3, 2017

ZIARA YA NAIBU WAZIRI MHANDISI MASAUNI NA WAZIRI BARANDAGIYE WA BURUNDI KATIKA KAMBI ZA WAKIMBIZI NDUTA NA MTENDELI MKOANI KIGOMA

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza katika mkutano wa hadhara na wakimbizi wa Burundi wanaoishi katika kambi za Nduta na Mtendeli, mkoani Kigoma, ikiwa ni ziara ya kikazi kukagua zoezi la urejeshwaji wa wakimbizi hao katika nchi yao. Katika ziara hiyo Naibu Waziri aliongozana na Waziri wa Mambo ya Ndani na Mafunzo ya Uzalendo kutoka serikali ya Burundi, Pascal Barandagiye (hayupo pichani)
Waziri wa Mambo ya Ndani na Mafunzo ya Uzalendo kutoka serikali ya Burundi, Pascal Barandagiye, akizungumza katika mkutano wa hadhara na wakimbizi wa Burundi wanaoishi katika kambi za Nduta na Mtendeli, mkoani Kigoma, ikiwa ni ziara ya kikazi kukagua zoezi la urejeshwaji wa wakimbizi hao katika nchi yao

wakimbizi wa Burundi wanaoishi katika kambi za Nduta na Mtendeli, mkoani Kigoma wakinyoosha mikono juu baada ya kuulizwa wangapi wanataka kurudi nchini kwao na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani), katika mkutano wa hadhara ikiwa ni ziara ya kikazi ya naibu waziri kukagua zoezi la urejeshwaji wa wakimbizi hao katika nchi yao

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na Waziri wa Mambo ya Ndani na Mafunzo ya Uzalendo kutoka serikali ya Burundi, Pascal Barandagiye (kulia), wakipiga ngoma baada ya kuwasili katika uwanja ulipofanyika mkutano wa hadhara uliowahusisha wakimbizi wa Burundi wanaoishi katika kambi za Nduta na Mtendeli, mkoani Kigoma. Ziara hiyo lengo lake ni kukagua zoezi la urejeshwaji wa wakimbizi hao katika nchi yao

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na Waziri wa Mambo ya Ndani na Mafunzo ya Uzalendo kutoka serikali ya Burundi, Pascal Barandagiye (kulia), wakiagana baada ya kumaliza kuzungumza na wakimbizi wa Burundi wanaoishi katika kambi za Nduta na Mtendeli, mkoani Kigoma. Ziara hiyo lengo lake ni kukagua zoezi la urejeshwaji wa wakimbizi hao katika nchi yao.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na wakimbizi wa Burundi wanaoishi katika kambi za Nduta na Mtendeli, mkoani Kigoma, baada ya kumalizika kwa mkutano wa hadhara ikiwa ni ziara ya kikazi kukagua zoezi la urejeshwaji wa wakimbizi hao katika nchi yao.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi


IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad