HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 14, 2017

VIWANGO VYA FIDIA VINAWEZA KUTOFAUTIANA BAINA YA MTU NA MTU LICHA YA KUFANANA ULEMAVU; DKT. MHINA

  NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Mbeya
VIWANGO vya madhara ya kuumia vinahusika sana katika kufikia matokeo ya tathmini anayofanyiwa mfanyakazi aliyeumia mahala pa kazi, Daktari bingwa mbobezi wa mifupa na viungo nchini, Dkt. Robert Mhina, (pichani juu), amesema.
Dkt. Mhina ameyasema hayo wakati akiwasilisha mada juu ya misingi inayopaswa kuzingatiwa na daktari au mtoa huduma ya afya wakati akimfanyia tathmini mfanyakazi aliyeumia mahala pa kazi, kwenye mafunzo ya siku tano yaliyoandaliwa na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), ili kuwajengea uwezo madaktari na watoa huduma za afya kutoka mikoa ya nyanda za juu Kusini yanayoendelea kwenye ukumbi wa Benjamin Mkapa jijini Mbeya.
Akifafanua Dkt. Mhina alisema, Viwango vya fidia vitatofautiana kulingana na viwango vya madhara aliyopata mtu kulingana na kazi anayofanya. “Mfano dereva aliyevunjika mguu ambao anautumia kukanyaga klachi na gia katika kazi yake, fidia yake haiwezi kulingana na mhudumu wa ofisi ambaye naye amevunjika mguu” Alisema na kufafanua kuwa.
“Dereva hawezi tena kuendelea na kazi yake ya udereva kwa vile hana mguu tena ambao aliutegemea kufanya kazi, lakini mhudumu anaweza kutumia gongo na akatembea, ingawa muda wa kufika mahala fulani katika ofisi utakuwa tofauti, lakini anaweza kuhamisha mafaili kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kwa maana hiyo bado ataendelea kufanya kazi hiyo tofauti na dereva.” Alisema
Kwa msingi huo, Dkt. Mhina ambaye pia ni mshauri wa masuala ya tiba alisema “Wananchi na wafanyakazi wanapaswa kujua kuwa mafao yatatolewa kutegemea na athari au kazi mtu anayofanya na hayawezi kufanana katika kupiga hesabu za kutoa mafao, kwani kuna vitu vya ziada vinapaswa kuzingatiwa pia.
Akifafanua zaidi kuhusi misingi hiyo ya ulipaji fidia, Mkurugenzi wa huduma za Tiba na Tathmini wa WCF, Dkt. Abdulsalaam Omar, alisema, zipo njia kadhaa zinazotumika kulipa fidia na kutaja baadhi yake kuwa ni fidia anayolipwa mfanyakazi aliyepata ulemavu baada ya kuumia,(impairment base approach) ambayo ndiyo inayotumika sasa kwa mujibu wa sheria katika kulipa fidia,  na nyingine ni ile kupoteza kipato kutokana na ulemavu wa kuumia mahala pa kazi, (wage loss approach)
“Unaweza ukapata ulemavu lakini bado kipato chako kiko pale pale, na kwa sheria za sasa ingawa bado kipato chako ni kile kile licha ya kuumia, na kwakuwa sheria ya fidia inatambua njia ile ya (Imparement base approach), basi mfanyakazi huyo atalipwa fidia”. Alisema Dkt. Omar.
Hata hivyo Dkt. Omar alisema, zipo nchi nyingine ambazo zinatumia mfumo huo wa pili wa mfanyakazi aliyeumia lakini kuumia huko hakupunguzi kipato chake, (wage loss), hawatoi fidia.


 Dkt. Mhina (kulia), na Dkt. Hussein, wakimsikiliza Dkt. Kishashu, wote hawa ni wawezeshaji wa semina hiyo.
 Dkt. Hussein Mwanga, akiwasilisha mada juu ya tathmini ya maradhi ya ngozi na kansa mahala pa kazi.
 Baadhi ya washiriki
  Baadhi ya washiriki
  Baadhi ya washiriki
 Mshiriki akizungumza
 Mshiriki akizungumza
 Afisa Mwandamizi anayeshughulikia madai ya fidia (Claims), Bw.Lembo, akizungumza
 Baadhi ya washiriki.
 Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusoianio WCF, Bi. Laura Kunenge, akizungumza.
 
Dkt. Mhina akitoa "somo" kwa washiriki.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad