HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, December 18, 2017

SERIKALI KUTOA MWONGOZO KURATIBU VITUO VYA WARAIBU WA DAWA ZA KULEVYA NCHINI.

 Mratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGO's) kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Bibi. Salome Mbonile akizungumza wakati wa hafla ya kusherehekea miaka minne tangu kuanzishwa kwa Kituo cha Upataji nafuu kwa watumiaji wa Dawa za Kulevya (PEDDEREF) kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni Msimamizi wa Programu wa Kituo hicho Khamis Ajib Dimand  na Mkurugenzi na Mwanzilishi wa kituo hicho Bi. Nuru Salehe Ahmed.
 Mkurugenzi na Mwanzilishi wa kituo hicho Bi. Nuru Salehe Ahmed akizungumza wakati wa hafla ya kusherehekea miaka minne tangu kuanzishwa kwa Kituo cha Upataji nafuu kwa watumiaji wa Dawa za Kulevya (PEDDEREF) kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni Msimamizi wa Programu wa Kituo hicho Khamis Ajib Dimand  na Mratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali(NGO's) kutoka   Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Bibi. Salome Mbonile (katikati).
 Mmoja wa wanufaika wa Kituo cha upataji nafuu kwa watumiaji wa dawa za kulevya (PEDDEREF) kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam Bi. Amina Mbonde akitoa ushuhuda namna alivyofanikiwa kuacha matumizi ya dawa za kulevya  wakati wa hafla ya kusherehekea miaka minne tangu kuanzishwa kwa kituo hicho jana. Kutoka kulia ni Mkurugenzi na Mwanzilishi wa kituo hicho Bi. Nuru Salehe Ahmed, Msimamizi wa Programu wa Kituo hicho Khamis Ajib Dimand  na Mratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGO's) kutoka   Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Bibi. Salome Mbonile na Msimamizi wa Programu wa Kituo hicho Khamis Ajib Dimand. 
 Msimamizi wa Programu wa Kituo hicho Khamis Ajib Dimand akielezea jambo wakati wa hafla ya kusherehekea miaka minne tangu kuanzishwa kwa Kituo cha upataji nafuu kwa watumiaji wa Dawa za Kulevya (PEDDEREF) kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kulia ni Mkurugenzi na Mwanzilishi wa kituo hicho Bi. Nuru Salehe Ahmed na Mratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGO's) kutoka   Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Bibi. Salome Mbonile (katikati).
 Mratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGO's) kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Bibi. Salome Mbonile(wapili kushoto) akishiriki zoezi la kukata keki wakati wa hafla ya kusherehekea miaka minne tangu kuanzishwa kwa Kituo cha upataji nafuu kwa watumiaji wa Dawa za Kulevya (PEDDEREF) kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni Mmoja wa wanufaika wa Kituo hicho Bi. Amina Mbonde,Mkurugenzi na Mwanzilishi wa kituo hicho Bi. Nuru Salehe Ahmed na Afisa Habari toka Ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Nyanzobe Magalle.
 Mratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGO's) kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Bibi. Salome Mbonile(wapili kushoto) akimlisha keki Mmoja wa wanufaika wa Kituo cha upataji nafuu kwa watumiaji wa Dawa za Kulevya (PEDDEREF) kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam Bi. Amina Mbonde wakati wa hafla ya kusherehekea miaka minne tangu kuanzishwa kwa kituo hicho jana. Kulia ni Mkurugenzi na Mwanzilishi wa kituo hicho Bi. Nuru Salehe Ahmed.


Na Mwandishi Wetu
SERIKALI kupitia Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Nchini (DCEA) imesema ipo mbioni kutoa mwongozo wa kuratibu na kusimamia viwango vinavyowiana vinavyotarajiwa kutumika katika Vituo  vyote vya Upataji nafuu kwa watumiaji wa dawa za kulevya nchini.
Hayo yamesemwa jana Jijini Dar es Salaam na Mratibu wa Mashirika yasiyo ya Serikali NGO’s kutoka (DCEA), Salome Mbonile wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka minne ya kituo cha upataji nafuu kwa watumiaji wa dawa za kulevya (PEDDEREF) kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam.
Mbonile alisema katika kuhakikisha kuwa mwongozo huo unaleta tija iliyokusudiwa, Serikali inatarajia kuwashirikisha wadau wote katika mapambano dhidi ya madawa ya kulevya ili waweze kutoa mapendekezo, ushauri na maoni ili kuweza kuisaidia jamii hususani makundi ya vijana katika kujiepusha na matumizi ya madawa ya kulevya.
"Kumekuwa na uwoga kwa wananjamii kutembelea Sober House (Nyumba za upataji nafuu kwa watumiaji wa madawa ya kulevya, lakini kupitia mwongozo huu tunataka kuweza viwango vinavyofanana ili kutoa fursa kwa watu wote kutembelea makazi haya" alisema Mbonile.
Mbonile alisema mapambano ya vita dhidi ya matumizi ya madawa ya kulevya nchini hayana budi kuungwa mkono na wadau mbalimbali wa maendeleo na hivyo Serikali itaendelea kutoa ushirikiano wa na asasi, taasisi mbalimbali ili kuhakikisha kuwa jamii ya Kitanzania hususani vijana inaendelea kuwa salama na kuondokana na matumizi ya dawa za kuelvya.
Aliongeza kuwa hadi sasa Tanzania ina jumla ya Nyumba za upataji nafuu kwa watumiaji wa dawa za kulevya 25 pamoja na Asasi 16 zinazotoa elimu na kuhamasisha jamii kutambua madhara mbalimbali yatokanayo na matumizi ya dawa za kulevya ikiwemo hatari ya maambuzi ya magonjwa mbalimbali pamoja na vifo.
Aidha aliongeza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii yenye malengo ya kupambana na matumizi ya dawa za kulevya nchini, hatua inayolenga kuwaunga mkono na kuendelea kutoa ushirikiano wa karibu kwa kadri inavyowezekana.
“Nyumba za upataji nafuu kwa watumiaji wa dawa za kulevya nyingi zinajengwa na waliowahi kutumia dawa za kulevya na Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za mashirika haya na kutoa ushirikiano unaohitajika ili kuviweza kutekeleza vyema majukumu yake” alisema Mbonile.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa PEDDEREF, Nuru Ahmed alisema suala la matumizi ya dawa za kulevya limekuwa kubwa hususani kwa makundi ya vijana na kuwataka wazazi kushikamana kwa pamoja badala ya kutupiana lawama pindi mtoto anapoanza kujihusisha na matumizi ya dawa za kulevya.
Alisema kuwa ujenzi wa malezi mapya ya vijana walioacha matumizi ya dawa za kulevya, yanawezeakana iwapo wadau wote hususani jamii zitajihusisha katika kukemea unyanyapaa ambao umekushika kazi katika jamii, hatua inayochangia kufifisha jitihada zinazofanywa na Serikali na mashirika mbalimbali nchini.
“Kituo chetu kina jumla ya walaibu 58 wakiwemo wanawake 16 na wanaume 42, tunashukuru kwa ushirikiano tunaoupata kutoka kwa Serikali na kuwaomba wadau wengine waendelee kushirikiana katika kujenga jamii salama kwa mustakabali wa kizazi chetu” alisema Nuru.
Naye Mraibu aliyepata nafuu katika utumiaji wa dawa za kuelvya, Amina Mbonde alisema alitumia nusu ya uhai wa maisha yake katika kupambana kuachana na matumizi ya dawa za kulevya, na kukipongeza kituo cha PEDDEREF kutokana na mwamko wake wa kuwaweka pamoja walaibu wa madawa ya kulevya na kuwaonyesha mwanga mapya wa maisha yao.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad