HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, December 1, 2017

MKOA WA NJOMBE WAONGOZA KWA MAAMBUKIZI YA UKIMWI

Mkoa wa Njombe umetajwa kuongoza kuwa na asilimia 11.4 ya watu wanaishi na virusi vya Ukimwi huku Zanzibar wanaoishi na virusi hivyo ni chini ya asilimia 1.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk Albina Chuwa ametoa takwimu hizo leo Desemba 1 katika maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani ambayo Kitaifa imefanyika viwanja vya Mnazi Mmoja.
Dk Chuwa amesema mkoa wa Lindi umekuwa wa mwisho kwa watu wenye virusi vya ukimwi na idadi ya asilimia 0.1 huku maambukizo kwa Jiji la Dar es Salaam yamepungua hadi kufikia asilimia 4.7 ikiwa na maana watu 133,971 wanaishi na ugonjwa huo.
Mkurugenzi huyo amesema kwa ujumla watu 1.4 milioni nchini Tanzania wanaishi na virusi vya Ukimwi na takwimu hizo ndiyo rasmi hivyo asitokee mtu au kikundi cha watu kupotosha.
"Nasema kwa sababu kuna watu wanakurupuka na kuja na takwimu zao. Naomba watambue takwimu ni fani kama fani nyingine na zina miiko yake," amesema Dk Chuwa
Hata hivyo, Dk Chuwa amesema Serikali haimzuii mtu au kikundi kufanya utafiti ila ni lazima awasiliane na ofisi ya takwimu wapitie dodoso zake kabla ya kuruhusiwa kufanya.
Amesema atakayekiuka na kupotosha takwimu adhabu yake iliyowekwa kisheria ni kifungo cha miaka mitatu au faini Sh10 milioni au vyote kwa pamoja.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi, Justin Mwinuka ameiomba Serikali kutengeneza Sheria zitakazoratibu upatikanaji wa dawa za kufubaza makali ya ukimwi (ARV).
Mwinuka amesema uwepo wa sheria hiyo utasaidia kuwabana watu wanaofanya biashara kupitia dawa hizo.Amesema wagonjwa wengi hawapati dawa kutokana na kushindwa kumudu gharama.
"Tuna changamoto ya uhaba wa dawa na zinazopatikana zinauzwa sasa wagonjwa wanashindwa kupata fedha za kununua,"
Mwinuka pia ameomba watu wanaoishi na virusi vya ukimwi kuingizwa kwenye mpango wa kaya maskini Tasaf ili waweze kutatua changamoto ya uhakika wa lishe.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad