HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, December 19, 2017

BARAZA LA WATOTO TAIFA LATOA ELIMU YA MATUMAINI KWA WATOTO WA MITAANI

 Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Watoto Taifa wakishiriki kufanya usafi katika  kituo cha kulelea watoto wa mitaani cha Amani Street Children Centre kilichopo katika Manispaa ya Singida.
 Mwenyekiti wa Baraza la Watoto Taifa, Joel Festo akikabidhi zawadi ya Vyandarua kwa Mratibu wa   kituo cha kulelea watoto wa mitaani cha Amani Street Children Centre kilichopo katika Manispaa ya Singida.
 Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Watoto Taifa wakiwa katika picha ya pamoja na watoto wa  kituo cha kulelea watoto wa mitaani cha Amani Street Children Centre kilichopo katika Manispaa ya Singida.
Mkurugenzi  wa Idara ya Watoto Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Bi. Margaret Mussai  akikabidhi zawadi ya Vyandarua kwa Mratibu wa   kituo cha kulelea watoto wa mitaani cha Amani Street Children Centre kilichopo katika Manispaa ya Singida.

Na Anthony Ishengoma
Wajumbe  wa Balaza  la Watoto  la Taifa leo wameungana na watoto wanaotunzwa katika kituo cha kulelea watoto wa mitaani Amani kilichopo katika Manispaa ya Singida ili kuwafariji na kuwapatia elimu juu ya umuhimu wa kuishi katika familia kama ilivyo kwa watoto wengine wanaoishi na wazazi  wao.

Watoto  hao wanalelewa katika kituo hicho baada yakuwa wamejiingiza mjini na kuanza maisha kabla ya wakati jambo  ambalo uwalazimisha kuishi katika mazingira hatarishi ikiwemo  wizi na kuvutishwa bangi na madawa ya kulevya.

Mkuu wa kituo cha kulelea watoto hao katika kituo cha Amani Street Children centre Bi. Getruda Kifumu ametaja chanzo cha kuongezeka kwa watoto wa mitaani kuwa ni umasikini wa kipato katika familia, ugonvi katika ndoa, kuachana kwa familia ikiwemo imani potofu ya kuwa mjini kuna nafuu  ya maisha.

Aidha Bi. Getruda amesema kituo chake kina zaidi ya watoto 50 ambao tayari wamerudishwa kwa familia baada ya kuwa wamezungumza na familia lakini pia na watoto wenyewe japokuwa baadhi ya watoto utoroka.

Amesema kituo kinakaa na watoto kwa miezi tisa na baada ya hapo  uwarudisha kwa familia zao na kuendelea na maisha na kukukiri kuwa baadhi ya watoto uweza kurejea  mitaani na kulazimika  kurudishwa kituoni hapo.

Bi Getruda ameongeza kuwa changomoto iliyopo ni kuwa watoto wengine wanakuwa na umri mkubwa hivyo kupata changomoto ya kuwarudisha katika mfumo rasmi wa shule na sababu inayowafanya baadhi yao  wasiendelee kimasomo.

Mkurugenzi  wa Idara ya Watoto  Nchini Bi. Margaret Mussai ameviambia vyombo vya kuwa utafiti wa shirika la  kimataifa la watoto UNCEF wa mwaka 2016 unasema Tanzania ina watoto elfu35 wanaoishi katika mazingira hatarishi.

Amezija sababu za kuwepo  hali hiyo hapa Nchini kuwa ni watoto kukosa malezi bora toka kwa familia zao kwa kuwa utafiti pia unaonesha asilimia 60 ya vitendo  vya ukatiri vinatokana na familia za Watoto  akitaja  vitendo  vya kulawiti watoto vimeripotiwa kuhusisha ndugu  wa karibu na watoto.

Amezitaja sababu nyingine kuwa umasikini na wazazi  kuangaika zaidi kutafuta fedha na kusahau majukumu ya kulea watoto wao jambo linalopelekea watoto kuiga kila jambo kutoka  mitaani badala ya kupewa miongozo ya maisha na wazazi  wao.

Mkutano wa Baraza  la Watoto  Taifa unaendelea leo mjini Singida agenda kubwa  ikiwa ni kufanya uchaguzi wa wawakilishi wawili watakao liwakilisha Taifa katika mkutano wa kimataifa wa watoto utakaofanyika mapema mwakani Nchni Sweden.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad