HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, November 14, 2017

TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA YATEMBELEA MAKAZI YA WAZEE WASIOJIWEZA NA KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA MKOANI SHINYANGA

 Katibu Msaidizi Tume ya Kurekebisha Sheria Agnes Mgeyekwa akiongea na Wazee pamoja na wafanyakazi wa makazi ya wazee wasiojiweza ya Kolandoto yaliyopo katika manispaa ya Shinyanga wakati Tume ilipotembelea makazi hayo ikiwa ni sehemu ya Utafiti wa Mfumo wa Kisheria wa Huduma za Ustawi wa Jamii Tanzania.
 Sehemu ya wazee wa Makazi ya Wazee wasiojiweza ya Kolandoto yaliopo katika Manispaa ya Shinyanga wakimsikiliza katibu Msaidzi Tume ya Kurekebisha Sheria Bi. Agnes Mgeyekwa.
 Mkuu wa Makazi ya Wazee wasiojiweza ya Kolandoto katika manispaa ya Shinyanga Bi. Sophia Kang’ombe akisisitiza jambo wakati Tume ya Kurekebisha Sheria ilipotembelea makazi hayo wakati wa utafiti wa Mfumo wa Kisheria wa Huduma za Ustawi wa Jamii nchini.
 Mhadhiri Msaidizi kutoka chuo cha Ustawi wa Jamii Bw. Paul Mwangosi akizungumza wakati Tume ya Kurekebisha Sheria ilipotembelea Makazi ya Wazee wasiojiweza  ya Kolandoto.
 Katibu Msaidizi  Tume ya Kurekebisha Sheria Bi. Agnes Mgeyekwa akimuelezea Kaimu Katibu Tawala wa mkoa wa Shinyanga Bw. Alfred Shayo  lengo la Tume kufanya utafiti kuhusu Mfumo wa Kisheria wa Huduma za Ustawi wa Jamii Tanzania.
 Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga Bw. Alfred Shayo akizungumza na ujumbe wa Tume ya Kurekebisha Sheria ulipomtembelea ofisini kwake.
 Katibu Msaidizi Tume ya Kurekebisha Sheria Bi. Agnes Mgeyekwa akimkabidhi  Kaimu Katibu Tawala wa mkoa wa Shinyanga Bw. Alfred Shayo  baadhi ya Ripoti zilizofanyiwa kazi na Tume
 Mmoja wa Wazee katika Makazi ya Wazee wasiojiweza ya kolandoto  katika Manispaa ya Shinyanga Bw. Zengo Masemba akizungumza wakati ujumbe wa Tume ya Kurekebisha Sheria ulipotembelea Makazi ya Wazee hao mkoani Shinyanga.  
 Mmoja wa wazee katika makazi ya Kolandoto Zengo Masemba akifurahia kwa kucheza na ujumbe wa Tume  na maofisa wengine wakati ujumbe wa Tume ya Kurekebisha Sheria ulipotembelea makazi yao wakati wa kufanya utafiti kuhusu Mfumo wa Kisheria wa Huduma za Ustawi wa Jamii Tanzania katika mkoa wa Shinyanga
 Katibu Msaidizi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Bi Agnes Mgeyekwa  na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja  na wazee pamoja na wafanyakzi wa makazi ya wazee wasiojiweza ya Kolandoto yaliyopo katika manispaa ya Shinyanga mkoa wa Shinyanga
 Mkurugenzi wa  kituo cha kulelea watoto yatima cha ‘Shinyanga Society for Orphans’ bi. Ayam Ally Said akizungumza na ujumbe wa Tume ya kurekebisha Sheria uliokwenda kutembelea kituo hicho wakati wa kufanya utafiti kuhusu mfumo wa kisheria wa Huduma za Ustawi wa Jamii Tanzania.
 Katibu Msaidizi Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Bi. Agnes Mgeyekwa akiwa na Watoto wanaolelewa katika Kituo cha Watoto yatima cha ‘Shinyanga Society for Orphans’ kilichopo mkoani Shinyanga
 Katibu Msaidizi Tume ya Kurekebisha Sheria bi. Agnes Mgeyekwa akiangalia  baadhi ya magodoro yaliyotolewa msaada kwa Kituo cha Kulelea watoto yatima cha ‘Shinyanga Society for Orphans’  wakati Tume ikifanya Utafiti kuhusu Sheria ya Huduma za Ustawi wa Jamii katika mkoa wa Shinyanga, anayemuonesha ni Mkurugenzi wa kituo hicho bi. Ayam Ally Said
Eneo la makazi ya Wazee wasiojiweza ya Kolandoto katika manispaa ya Shinyanga mkoa wa Shinyanga

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad