HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, November 19, 2017

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Taasisi ya Kimataifa ya Kiislamu ya Misaada (IIRO) zakamilisha kambi ya siku nne ya upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization)

Mufti Sheikh Abubakari Zubeir bin Ally akimkabidhi tuzo ya shukrani Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi wakati wa hafla fupi ya kumaliza kambi ya siku nne ya upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab iliyofanywa na Taasisi hiyo kwa kushirikiana na Taasisi ya Kimataifa ya Kiislamu ya Misaada (IIRO) ya nchini Saudi Arabia. Kushoto ni Balozi wa Saudi Arabia Nchini Mhe. Mohamed bin Mansour Al Malik.
Balozi wa Saudi Arabia Nchini Mhe. Mohamed bin Mansour Al Malik akimkabidhi tuzo ya shukrani Mufti Sheikh Abubakari Zubeir bin Ally katika hafla fupi ya kumaliza kambi ya siku nne ya upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab iliyofanywa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Taasisi ya Kimataifa ya Kiislamu ya Misaada (IIRO) ya nchini Saudi Arabia. Jumla ya wagonjwa 33 walifanyiwa upasuaji katika kambi hiyo.
Kaimu Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Dkt. Doroth Gwajima akiishukuru Serikali ya Saudi Arabia kupitia Taasisi ya Kimataifa ya Kiislamu ya Misaada (IIRO) ya nchi hiyo kwa kutuma wataalamu wake hapa nchini kutoa huduma ya upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab iliyofanyika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Jumla ya wagonjwa 33 walifanyiwa upasuaji katika kambi hiyo.
Madaktari bigwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Taasisi ya Kimataifa ya Kiislamu ya Misaada (IIRO) ya nchini Saud Arabia wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza kufanya upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab kwa wagonjwa 33.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad