HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, November 18, 2017

TAASISI YA DORIS MOLLEL YAZINDUA FILAMU MTOTO "NJITI" JIJINI DAR

Mgeni Rasmi katika hafla ya uzinduzi wa filamu fupi ya "Njiti", Waziri wa Madini, Angella Kairuki (katikati) akiwa na Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jaseem Al Najem (kulia) pamoja na Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel (DMF) na Balozi wa Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati "Njiti", Doris Mollel baada ya kukata utepe kuashiria uzinduzi huo, uliofanyika katika ukumbi wa sinema wa Cinemax, Dar Free Market, jijini Dar es salaam leo. Filamu hiyo ambayo inaelezea maisha ya Mtoto aliyezaliwa kabla ya wakati "Njiti" imeandaliwa na Taasisi ya Doris Mollel, imelenga kutoa elimu ya uelewa wa namna ya malezi bora kwa mtoto anayezaliwa kabla ya wakati. Uzinduzi huo umefanikiwa kwa ushirikiano wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Coastial Aviation, Slide Visual, Ashtom Media, Cinemax.
Mgeni Rasmi katika hafla ya uzinduzi wa filamu fupi ya "Njiti", Waziri wa Madini, Angella Kairuki akitoa hotuba yake, ambapo alitoa pongezi nyingi kwa Taasisi ya Doris Mollel kwa kufanikisha kupatikana kwa elimu ya uelewa wa namna ya malezi bora kwa mtoto anayezaliwa kabla ya wakati kupitia filamu hiyo.
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jaseem Al Najem akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa filamu fupi ya "Njiti", ambayo inaelezea maisha ya Mtoto aliyezaliwa kabla ya wakati "Njiti" iliyoandaliwa na Taasisi ya Doris Mollel, imelenga kutoa elimu ya uelewa wa namna ya malezi bora kwa mtoto anayezaliwa kabla ya wakati.
Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel (DMF) na Balozi wa Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati "Njiti", Doris Mollel akizungumza katika hafla hiyo, iliyofanyika katika ukumbi wa sinema wa Cinemax, Dar Free Market, jijini Dar es salaam leo. 
Sehemu ya wageni waliohudhulia hafla hiyo.

 Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jaseem Al Najem akimuonyesha
Waziri wa Madini, Angella Kairuki, moja ya mashine maalum za kuwasaidia kupumua Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati "Njiti" zilizotolewa na Ubalozi wa Kuwait kwa Taasisi ya Doris Mollel ili ziweze kuwafikia walengwa waliokusudiwa, muda mfupi baada ya kufanyika uzinduzi wa filamu fupi fupi ya "Njiti", ambayo inaelezea maisha ya Mtoto aliyezaliwa kabla ya wakati "Njiti" iliyoandaliwa na Taasisi ya Doris Mollel, imelenga kutoa elimu ya uelewa wa namna ya malezi bora kwa mtoto anayezaliwa kabla ya wakati. Kulia ni Muanzilishi wa Taasisi hiyo na Balozi wa Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati "Njiti", Doris Mollel.

 Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jaseem Al Najem akikabidhi moja ya msaada wa mabeseni ya Watoto kwa Waziri wa Madini, Angella Kairuki.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad