HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, November 10, 2017

SPIKA JOB NDUGAI AZUNGUMZA NA WABUNGE WALIOSHIRIKI MAFUNZO NCHINI CHINA.

 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioshiriki mafunzo ya kuwajengea uwezo wa utendaji wao wa kazi nchini China katika kikao kilichofanyika leo ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akipokea zawadi aliyopewa na Chuo Kikuu cha Guangdong  kilichopo Jijini Guangzhou China, wakati wa ziara ya Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini China, zawadi hiyo ilikabidhiwa na kiongozi wa Msafara , Mheshimiwa. Augustino Masele (kushoto) na wengine ni Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioshiriki mafunzo ya kuwajengea uwezo wa utendaji wao wa kazi nchini China katika tukio lililofanyika leo ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.
 Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakimsikiliza Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati) wakati wa kikao kilichofanyika leo katika ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Kiongozi wa Msafara, Mheshimiwa Augustino Masele (kushoto) iliyotoka Chuo Kikuu cha Guangdong  kilichopo Jijini Guangzhou China, wakati wa ziara ya Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini China, katika tukio lililofanyika leo ukumbi wa Spika Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (watatu kulia mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioshiriki mafunzo ya kuwajengea uwezo wa utendaji wao wa kazi nchini China katika tukio lililofanyika leo ukumbi wa Spika Mjini Dodoma. (PICHA NA OFISI YA BUNGE)​

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad