HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 2, 2017

RC MAKONDA AZINDUA UJENZI WA OFISI ZA WALIMU 402 JANA JIJINI DAR


Mkuu wa Mkoa Paul Makonda akiashiria kuzinduliwa kwa zoezi la ujenzi wa Ofisi za kisasa 402 za Walimu Mkoa wa Dar es Salaam ambapo amesema kukamilika ujenzi huo kutasaidia kuinua kiwango cha elimu mkoa hapo.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ,amezindua zoezi la ujenzi wa Ofisi za kisasa 402 za Walimu Mkoa wa Dar es Salaam ambapo amesema kukamilika ujenzi huo kutasaidia kuinua kiwango cha elimu mkoa hapo na kuongeza kuwa ujenzi wa Ofisi utafanka kwa haraka, chini ya Vijana wenye morali ya kazi kutoka JKT, Magereza na Jeshi la Polisi.

Ramani ya ofisi hizo inaonyesha kuwa na Ofisi ya Mwalimu Mkuu, Mwalimu Mkuu Msaidizi, Ofisi ya Walimu wa kawaida, Mhasibu, Karani, Chumba cha kuhifadhi Mitihani, Vyoo vya kisasa, Stoo, Jiko, Chumba cha Mikutano na sehemu kuweka Mafaili ambapo ndani ya ofisi zitafungwa AC, Feni, Samani, Taa za kisasa na Umeme.

Akizungumza Katika uzinduzi huo ulioenda sambamba na upandaji wa Miti RC Makonda amesema kuwa lengo la ujenzi huo ni kuwezesha Walimu kufanyakazi katika Mazingira mazuri yatakayowapa morali na hamasa ya kufundisha Wanafunzi.

Sanjali na hayo Makonda amewapongeza Walimu wa shule za msingi kwakuwezesha Mkoa wa Dar es salaam kushika nafasi ya kwanza kitaifa katika matokeo ya mtihani wa Darasa la saba ukilinganisha na nafasi ya nne waliyo pata mwaka jana na amewaomba kutoichia nafasi hiyo , pia walimu wa shule za sekondari nao wajitahidi ili waongoze katika matokeo ya mtihani kitafa.

"Rais ,ameshatuonyesha dira kwa kutoa elimu bure na sisi wasaidizi wake ni lazima tuendeleze maono yake, mimi sio kiongozi wa kusubiri kuagizwa ndio nifanye kazi kama ilivyo kwa Remote hadi ibonyezwe ndio ifanye kazi, mimi ni kiongozi wa kujiongeza, sijachaguliwa kuwa mzigo kwa serikali bali kuleta matumaini kwa wananchi"alisema.

Amewataka Viongozi kuacha Siasa kwenye mambo ya Msingi yanayolenga kuleta maendeleo kwakuwa Maendeleo hayana chama wala ubaguzi wa Dini."walimu hawa wanapowafundisha watoto wetu hawawaulizi vyama vyao wala dinizao tena watoto wenyewe hawa hawana vyama naombambeni ndugu zangu tuwe wamoja katika mambo ya maendeleo ,nashangaa kuna Wilayamoja wao hawatamani jambo jema nikupinga tu ,madai yao eti watanipa kiki,mmi sitafuti kiki nafanya kazi".

Awali mkuu wa wilaya ya Ilala  Sophia Mjema akizungumza wakati wa ukaribisho amemshukuru Rc Makonda kwa moyo wake wa kuwajali walimu kwa kuona shida yayao na kuahidi kufanya naye kazi begakwabega i kuendelea kutatua kero za wali na wananchi kwa ujumla ,Uzinduzi huo umehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Kamanda wa Polisi kanda maalumu Dar es Salaam Lazalo Mambosasa, Kamati ya Ujenzi wa Ofisi za Walimu, Maafisa Elimu, Wakuu wa Shule ,Diwani, Pamoja na wanachikutoka maeneo mbalimbali ya wilaya Ilala.

Naye Diwani wa kataya Majohe Mwenyevyake Waziri amepongeza hatua ya mkuu wa koa wa Dar es salaam kwa juhudi anazozifanya katika shuguli za maendeleo na kusema kuwa anamuuga mkono aendelee mbele zaidi.

"kwakweli hatamimi ilikuwa ni shauku yangu kuona walimu wakifanya kazi katika mazingira mazuri wanakuwa naofisi nzuri na anachokifanya Makonda kitukizuri napia kama kiongozi wa serila anatimiza wajibu wake mimi nimtakie kilalakheri" Alisema Waziri.

Nao baadhi ya wananchi walihudhuria uzinduzi huo wamesema weshukuru hatua hiyo na kusema kuwa walimu walikuwa wanadharirika ,walidharaulika walikuwa kamawametengwa ukienda ofisi za wizara zingne wanaofisi lakini wao walisahaulika sasa watafanya kazi kwa moyo kwakuwa watakuwa huru na maboyao .

Kwa upande wake Mwenyekti wa kamati ya ujenzi Canal Mbuge amewataka watanzani kuendelea kuchagia ujenzi huo ilikujenga mshikamano na utaifa kwa kujitolea katika mambo ya maendeleo na kuahidi kuwa wao kama wasimamizi wa ujenzi huo watahakikisha ujenzi huo unafanyika kwa ubora na viwango na kukamilika kwa wakati.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akilakiwa na baadhi ya viongozi wa majeshi pamoja na wakuu wa wilaya za mkoa wa Dar alipokwenda kuzindua zoezi la ujenzi wa Ofisi za kisasa 402 za Walimu Mkoa wa Dar es Salaam ambapo amesema kukamilika ujenzi huo kutasaidia kuinua kiwango cha elimu mkoa hapo.
Mku wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akikabidhiwa riasala iliyosomwa na mkuu wa shule ya msingiMajohe Grace Ndaro wakati wa uzinduzi wa zoezi la ujenzi wa Ofisi za kisasa 402 za Walimu Mkoa wa Dar es Salaam ambapo amesema kukamilika ujenzi huo kutasaidia kuinua kiwango cha elimu mkoa hapo
 Mkuu wa Mkoa Paul Makonda akizungumza na wananchi wa kata ya Majohe wakati wa uzinduzi wa zoezi la ujenzi wa Ofisi za kisasa 402 za Walimu Mkoa wa Dar es Salaam ambapo amesema kukamilika ujenzi huo kutasaidia kuinua kiwango cha elimu mkoa hapo
 Mkuu wa Mkoa Paul Makonda  akipanda mti.
Mkuu wa Mkoa Paul Makonda akiwa kazini kuashiria uzinduzi wa ujenzi za ofisi hizo ukiwa tayari umepamba moto.
Wananchi waliojitokeza.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad