HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, November 3, 2017

HOSPITALI YA AGA KHAN YAANZA KUTOA BURE HUDUMA YA UPANDIKIZAJI WA MATITI KWA AKINA MAMA

Hospitali ya Aga Khan imeanza kutoa bure huduma ya kupandikiza matiti kwa akina mama waliopatwa na magonjwa mbalimbali yaliyowapelekea kukatwa kwa kiungo hicho muhimu, ikiwemo wale waliokatwa kutokana na magonjwa ya Kansa, ukatili na kuungua moto.
Akizungumza na waandishi wa habari leo hii Jijini Dar es Salaam, Daktari bingwa wa kitengo cha upasuaji katika hospitali ya Aga Khan, Dr. Aidan Njau amesema huduma iliyoanza leo ni kuhudumia mgonjwa mmoja mmoja ili kusaidia wanawake wengi wenye matatizo hayo ambao wamekuwa wakiishi na maumivu makali hata kujisikia vibaya katika jamii .
“Kwa kuanzia tunaanza na wale wanawake waliokatwa matiti yao, tutatoa nyama kwenye sehemu yake ya mwili na kuipandikiza kwenye sehemu iliyokatwa na kuufanya muonekano wake urudi kama ulivyokuwa" amesema Dk. Njau.
Amesema huduma hiyo, itawafanya watanzania kushuhudia wanawake wakipandikizwa matiti jambo ambalo halijawahi kutokea hapa nchini na kuwaasa wanawake wenye matatizo hayo wajitokeze hospitalini hapo kwa wingi kwa ajili ya kupatiwa huduma hii ya bure.
Amesema, upasuaji huo utafanywa na madaktari wawili ambao ni Daktari bingwa wa kitengo cha upasuaji katika hospitali ya Aga Khan, Dr. Aidan Njau na Daktari bingwa Edwin Mrema kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili wote wakiwa na lengo la kurudisha furaha kwa wanawake wenye matatizo haya waliyokwisha ipoteza.
 Daktari bingwa wa upasuaji wa Hospitali ya Agakhan, Dkt Aidan Njau (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari juu ya huduma ya Upandikizaji wa Matiti kwa wanawake waliokatwa matiti kutokana na majanga mbalimbali ikiwemo karatani ya matiti kulia ni daktari bingwa wa upasuaji kutoka hospitali ya Taifa Muhimbili, Dkt Edwin Mrema. 
Dkt Edwin akiwa na baadhi ya wataalam wa magonjwa mbalimbali ya upasuaji

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad