Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe January
Makamba ameanza ziara ya kikazi ya siku saba visiwani Zanzibar. Katika siku ya
kwanza Mhe. Makamba amepata fursa ya kukutana na kufanya mazungumzo na
Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Zanzibar kwa lengo la kubadilishana uzoefu, kubaini
fursa na changamoto zinazowakabili na kuona namna bora ya kupata ufumbuzi.
Miongoni mwa changamoto zilizojadiliwa na kuwekewa mikakati ya utekelezaji ni pamoja
na masuala ya kodi, namna ya kunufaika kutoka na fursa zilizopo baina ya pande zote
mbili za Muungano na kuondoa vikwazo vinavyotokana na changamoto hizo ili kuleta
ufanisi.
Mhe. Makamba amewahakikishia wana juimuiya hao kuwa Ofisi yake itaratibu vikao kati
ya Ofisi yake na wafanyabiashara hao ili kupata fursa ya kutoa mrejesho wa utekelezaji
wa mambo waliyokubaliana.
Mbali ya kukutana na wafanyabiashara hao Waziri Makamba pia amepata fursa ya
kutembelea Vyombo mbalimbali vya Habari hapa Unguja kutoa ufafanuzi wa masuala
mbalimbali ya Muungano. Vyombo vilivyotembelewa ni pamoja na Zenji FM na Zenji Tv,
Bahari FM na Cocunut FM.
Ziara ya Waziri Makamba katika siku pili atatembelea Miradi mikubwa ya Mazingira na
kuwa na Vikao na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya Mapato
Zanzibar (ZRB).
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe January Makamba akizungumza na wanajumuiya ya Wafanyabiashara wa Zanzibar (hawapo pichani). Kikao
hicho kimefanyika hii leo eneo la Kinazini Zanzibar. Wengine katika picha ni viongozi wa Jumuiya hiyo.
Sehemu ya wafanyabiashara wa Zanzibar wanaounda Jumuiya ya Wafanya Biashara wa Zanzibar wakiwa
katika kikao na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe January
Makamba aliyewaalika kujumuika kubadilishana uzoefu na kuwaomba waainishe changamoto
zinazowakabili na kuona namna bora ya kuzipatia ufumbuzi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe January Makamba akisalimiana
na aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Muungano katika Serikali ya awamu ya nne Mhe.
Mohammed Seif Khatibu ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Zanzibar Media Coorporation, Waziri
Makamba alipata pia wasaa wa kufanya mahojiano katika chombo cha Habari cha Zenji FM na Zenji TV.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe January Makamba akifanya
mahojiano maalumu katika Kituo cha Redio cha Cocunut FM.
No comments:
Post a Comment