HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, October 28, 2017

Washindi wa Vipaji vya Sauti lafikia tamati jijini Dar, Kumi kwenda China

Washindi 25 wa shindano la vipaji vya sauti wakiwa kwenye fainali hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa LAPF jijini Dar es Salaam.


STARTIMES Tanzania kupitia chaneli yake ya Star Swahili hatimaye imemaliza shindano la kusaka vipaji vya sauti katika fainali iliyofanyika Ijumaa hii jijini la Dar es Salaam.
Shindano hili lilifanyika katika mikoa ya Mwanza na Dar es Salaam pamoja na Zanzibar na kupatikana washindi takribani 25 waliofuzu kuingia fainali. Washindi kumi wamepatikana ambao watakwenda kufanya kazi ya kuigiza sauti makao makuu ya Kampuni ya Startimes nchini China.

Akizungumza wakati wa Fainali hiyo Makamu wa Rais wa Startimes Tanzania, Zuhura Hanif  alisema Washindi wa mwaka jana wamepata nafasi ya kuhudhuria makongamano makubwa ya kuonyeshatamaduni mmablimbali likiwemo lile la One Belt One Road na kufanya onyesho la Kiswahili.Pia Shindano hili ni nafasi ya kukabiliana na tatizo la ajira kwani washindi wanaopatikana, moja kwa moja hupata nafasi ya Ajira makao makuu ya Kampuni ya Startimes nchini China.

Msanii maarufu nchini Tanzania Kutoka kundi la Orijino Komedi maarufu kama Mpoki a k a Muarabu wa Dubai(wa kwanza kulia) kizungumza jambo mara baada ya kutaja washindi 25 waliofuzu kuingia fainali ya shindano la Vipaji vya Sauti katika tamthiliya za kigeni kwa awamu ya pili ya mwaka 2017.
Majajji wa shindano la vipaji vya sauti la awamu ya pili  lililofanyika katika ukumbi wa LAPF jijini Dar es Salaam leo. Wa kwanza kishoto ni Msanii wa filamu nchini Jacob Stephen maarufu kama JB, kulia  Msanii wa muziki wa asili, Mrisho Mpoto pamoja na aliyekuwa mshindi wa shindano la vipaji vya sauti mwaka 2016/17.

Baadhi ya washiriki wa shindano la vipaji vya sauti msimu wa pili wa mshindano hayo yanayodhamuniwa na Startimes Tanzania wakionesha namna wanavyoweza kuigiza sauti kwenye fainali iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Msanii maarufu nchini Tanzania Kutoka kundi la Orijino Komedi maarufu kama Mpoki a k a Muarabu wa Dubai akizungumza jambo kwenye fainali ya shindano la kusaka vipaji lililofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia shindano la vipaji vya sauti msimu wa pili kwa mwaka 2017.
 Makamu wa Rais wa Startimes Tanzania, Zuhura Hanif akizungumza na waandishi wa habari wakati wa  shindano la vipaji vya sauti msimu wa pili mwaka 2017 lililofanyika katika ukumbi wa LAPF jijini Dar es Salaam.
Washindi 10 wa shindano la vipaji vya sauti walioshinda kwenda nchini China kufanya kazi makao makuu ya Kampuni ya Startimes  kwenye fainali hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa LAPF jijini Dar es Salaam.
 Mmoja wa washindi walioingia kumi bora akipokea zawadi ya simu ya Startimes kutoka kwa Makamu wa Rais wa Startimes Tanzania, Zuhura Hanif mara baada ya kumalizika kwa shindano la vipaji vya sauti msimu wa pili lililofanyika katika ukumbi wa LAPF jijini Dar es Salaam.
 Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA), Dkt. Seleman Sewangi(kulia) akimkabidhi zawadi ya Television ya Startimes mshindi wa kwanza wa shindano la vipaji vya sauti msimu wa pili, Coletha Raymond mara baada ya kuibuka mshindi wa shindano hilo.

Mshindi wa kwanza hadi wa tatu wa shindano la vipaji vya sauti msimu wa pili mwaka 2017 wakiwa kwenye picha ya Pamoja.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad