HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, October 26, 2017

NGUZO YA UMEME YADONDOKA MBEZI KWA MSUGULI.

Mvua inayoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam imesababisha adhaa kwa wakazi wa jiji hilo ambapo kwa maeneo ya Mbezi kuelekea Bwaloni/Kwa Msuguli au Malamba Mawili Shule nguzo ya umeme ya shirika la umeme la TANESCO imedondoka eneo la Malamba Mawili msikitini na kusababisha kufunga njia kwa wasafiri wa magari ambapo hakuna magari yanayovuka kwenda upande wa pili. 

Tanesco tunawaomba msaada tumekwama inasemekana imedondoka saa 9 Usiku kuamkia leo 26.10.2017.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad