HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 4, 2017

MKUU WA MAJESHI TANZANIA AWAONYA WATU WANAOTUMIA JINA LA JESHI HILO KUDANGANYA UMMA KWAMBA WANATOA AJIRA ZA JESHI

Mkuu wa Majeshi ya ulinzi Tanzania,Generali Venance Mabeyo amekemea na kutoa onyo kali kwa baadhi ya watu wanaotumia mwanvuli wa wastaafu wa jeshi,askari wa jeshi au nafasi ya vyeo vyao ndani na nje ya jeshi la wananchi Tanzania kwa kulaghai umma kwamba watoe fedha ili wawasaidie kupata ajira ndani ya jeshi hilo.

Mkuu wa Majeshi ya ulinzi Tanzania,Generali Venance Mabeyo alifika katika kituo cha ITV na kupokelewa na mkurugenzi wa ITV/Radio One Joyce Mhavile pamoja na viongozi wengine na kusaini kitabu cha wageni mashuhuri katika kituo hicho na kisha kutembelea katika maeneo vyumba mbalimbali vya kurushia habari. 

Akizungumza katika kipindi cha dakika 45 kinachorushwa na kituo cha ITV na Radio one kila jumatatu saa 3 usiku na marudio ni jumatano saa 7 kamili mchana,mkuu wa Majeshi ya ulinzi Tanzania,Generali Venance Mabeyo amesema jeshi lake haliwezi kuvumilia baadhi ya watu wenye nia mbaya ya kuchafua jeshi hilo kwa tabia yao mbaya ya kuchukua pesa ndani ya jamii kwa kujifanya watasaidia watu kupata ajira jeshini wakati jeshi la wananchi tanzania halina utaratibu wa kuajiri watu kwa kutumia njia hiyo na hivyo waache tabia hiyo mara moja.

Kwa undani wa mazungumzo na mkuu wa majeshi ya ulinzi nchini Generali Venance Mabeyo,usikose kuangalia kipindi cha dakika 45 jumatatu saa 3 usiku kupitia kituo chako bora cha ITV au kupitia Radio one Stereo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad