HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, October 26, 2017

KAMPUNI YA KILUWA INDUSTRIAL GROUP OF COMPANIES YAFANIKIWA KUANDAA KONGAMANO KUBWA LA UHAMASISHAJI WA UWEKEZAJI WA VIWANDA JIJINI BEIJING,CHINA



Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Mbelwa Kairuki akizungumza mbele ya Wamiliki wa Viwanda,Wafanyabiashara na makampuni mbalimbali wakati wa kufungua Kongamano kubwa la uwekezaji wa Viwanda lililofanyika jana Oktoba 25,2017 mjini Beijing,nchini China.Kongamano hilo kubwa lenye uhamasishaji mkubwa wa uwekezaji wa Viwanda nchini Tanzania,liliandaliwa na Kampuni ya Kiluwa Industrial Group of Companies.Picha Ahmad Michuzi-China.

Balozi Kairuki ameupongeza uongozi wa Kampuni ya Kiluwa Industrial Group of Companies kwa kuthubutu na kuonesha juhudi kubwa za kutafuta na kuwahamasisha washirika mbalimbali katika suala zima la uwekezaji wa viwanda nchini Tanzania.

Balozi Kairuki amesema kuwa,yeye yuko tayari kushiriki kwa pamoja kusaidia kuendelea kuwahamasisha Wawekezaji wa nchini China,kuja kuwekeza nchini Tanzania,ili kuhakkisha dhana ya Tanzania ya Viwanda inatimia na hatimaye nchi ya Tanzania kufikia uchumi wa kati kupitia viwanda.

"Kwa kufanya hivyo sote kwa pamoja tutakuwa tunetekeleza kwa vitendo,na pia kuunga mkono dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli ya kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi ya Viwanda",alisema Balozi Kairuki.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Kiluwa Industrial Group of Companies,Mohamed Said Kiluwa akizungumza mbele ya Wamiliki wa Viwanda,Wafanyabiashara na makampuni mbalimbali waliojitokeza kushiriki Kongamano la uwekezaji wa Viwanda lililofanyika jana Oktoba 25,2017 mjini Beijing,nchini China.Kongamano hilo kubwa lenye uhamasishaji mkubwa wa uwekezaji wa Viwanda nchini Tanzania,liliandaliwa na Kampuni ya Kiluwa Industrial Group of Companies.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Kiluwa Industrial Group of Companies,Mohamed Said Kiluwa akipongezwa mara baada ya kutoa hotuba yake .
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Kiluwa Industrial Group of Companies,Mohamed Said Kiluwa akiwalekeza jambo baadhi ya Wadau wenye nia ya Uwekezaji nchini Tanzania,mara baada ya Kongamano la uwekezaji wa Viwanda kumalizika.Kongamano hilo lilifanyika Oktoba 25,2017 katika moja ya ukumbi wa hotel ya King Wing,mjini Beijing nchini China,ambapo mgeni rasmi alikuwa Balozi wa Tanzania nchini humo,Mh Mbelwa Kairuki.
Katibu Tawala mkoa wa Pwani, Zuberi Samataba akijibu maswali mbalimbali yaliyokuwa yameulizwa na baadhi ya Washiriki wa Kongamano hilo la Uhamasishaji wa uwekezaji wa Viwanda nchini Tanzania,ndani ya moja ya ukumbi wa hotel ya King Wing mjini Beijing nchini China.Mh Semataba ambaye aliongozana na baddhi ya viongozi waandamizi wa Serikali mkoa wa Pwani,aliwahikikishia mazingira mazuri Washiriki hao wenye nia ya kuwekeza nchini Tanzania katika sekta mbalibali ikiwemo Viwanda,madini na kilimo na kuwa.
Kongamano la Uhamasishaji uwekezaji wa Viwanda kwa nchini Tanzania likiendelea mjini Beijing,nchini China.
Sehemu ya meza kuu na baadhi ya Washiriki wa kongamano hilo wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo.
Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Mbelwa Kairuki ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi akiwasili ukumbini kufungua kongamano la Uwekezaji wa Viwanda akifuatiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Kiluwa Industrial Group of Companies,Mohamed Said Kiluwa (wa pilia kulia) ambao ndio waandaaji wa kongamano hilo ambalo lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa
Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo la Uwekezaji wa Viwanda,wakifuatilia kwa makini yaliyokuwa yakjiri ukumbini humo,pichani kati ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Kiluwa Industrial Group of Companies,Naima Mohamed Kiluwa ambao ndio wameandaa kongamano hilo.
Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo la Uwekezaji wa Viwanda,wakifuatilia kwa makini yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Kiluwa Industrial Group of Companies,Naima Mohamed Kiluwa akizungumza jambo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kibaha Vijijini,Bi.Tatu Selemani.
Picha ya pamoja kutoka meza kuu na baadhi ya Wadau wakuu wa Kongamano hilo la Uwekezaji wa Viwanda.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad