Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na
Makamishna na Wakuu wa Vitengo vya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakati alipofanya ziara
Makao Makuu ya Jeshi hilo, jijini Dar es Salaam leo. Katika hotuba yake Masauni alilitaka Jeshi
hilo kutoa elimu zaidi kwa umma pamoja na kuongeza kasi ya ufunguaji wa vituo vya zimamoto
katika wilaya zote nchini. Kushoto ni Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, (CGF), Thobias
Andengenye, na kulia ni Kamishna wa Utawala na Fedha wa Jeshi hilo, Michael Shija.
Na Felix Mwagara (MOHA)
NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni
amelitaka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kuongeza kasi kufungua vituo vya
zimamoto katika wilaya zote nchini pamoja na kutoa elimu kwa umma juu ya
kinga na tahadhari ya majanga ya moto.
Akizungumza na Makamishna na Wakuu wa Vitengo katika Ukumbi wa Mikutano
wa Makao Makuu ya Jeshi hilo, Masauni alisema Serikali ya Awamu ya Tano
kusudio lake ni kuipeleka nchi katika uchumi wa kati na viwanda hivyo ili
maendeleo yapatikane lazima Jeshi hilo lijiimarishe zaidi.
“Akikisheni mna peleka maafisa wa zimamoto katika wilaya zote nchini ili
wakaweze kutoa elimu kwa umma jinsi ya kuzima moto, kwasababu kinga ni bora
kuliko tiba,” alisema Masauni.
Aidha, Masauni alisema zipo changamoto kadhaa zinazolikabili Jeshi hilo,
ikiwemo magari ya kuzimia moto hayatoshi, vifaa vya mahokozi pamoja na
ukosefu wa madawa ya kuzimia moto, lakini Serikali itajitahidi kuzitatua kadiri ya
uwezo wake.
Kwa upande wake Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, Thobias Andengenye, alisema
amepokea maelekezo hayo kutoka kwa Naibu Waziri, na kumuhakikishia kuwa,
Jeshi lake linaona ukuaji wa kasi wa viwanda nchini kunahitaji sana huduma
zitolewazo na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.
“Tunashukuru kwa ujio wako, maelekezo uliotupa tumeyapokea, tunakuhakikishia
kujipanga zaidi katika kuongeza nguvu zaidi katika kukabiliana na majanga ya
moto,” alisema Andengenye.
Hata hivyo, Andengenye aliiomba Serikali kuiongezean uwezo zaidi Jeshi hilo na
kuipatia vitendea kazi vya kisasa pamoja na kuongeza rasilimali watu ili kuipa
nguvu zaidi Jeshi hilo katika kutekeleza majukumu yake.
Masauni alifanya ziara hiyo ya siku moja kwa lengo la kuzungumza na viongozi
wa Jeshi hilo kuhusiana na mipango ya mbalimbali ya Serikali na Jeshi hilo kuhusu
kukabiliana na majanga ya moto nchini.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, (CGF), Thobias Andengenye akitoa taarifa
yake utendaji kazi wa Jeshi lake kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi
Hamad Masauni (katikati meza kuu), wakati kiongozi huyo alipofanya ziara ya kikazi Makao
Makuu ya Jeshi hilo, jijini Dar es Salaam leo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akimsikiliza
Mchumi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Boniface Mkumbo alipokua anafafanua mipango
mbalimbali ya kuliendeleza jeshi hilo. Kulia kwa Naibu Waziri ni Kamishna Jenerali wa Jeshi
hilo, (CGF), Thobias Andengenye. Katika hotuba yake kwa viongozi wa Jeshi hilo, Masauni
alilitaka Jeshi hilo kutoa elimu zaidi kwa umma pamoja na kuongeza kasi ya ufunguaji wa vituo
vya zimamoto katika wilaya zote nchini.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na
Makamishna na Wakuu wa Vitengo vya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakati alipofanya ziara
Makao Makuu ya Jeshi hilo, jijini Dar es Salaam leo. Katika hotuba yake Masauni alilitaka Jeshi
hilo kutoa elimu zaidi kwa umma pamoja na kuongeza kasi ya ufunguaji wa vituo vya zimamoto
katika wilaya zote nchini. Kulia kwa Naibu Waziri ni Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo, (CGF),
Thobias Andengenye. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
No comments:
Post a Comment