HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, October 5, 2017

DED MKURANGA AWASILISHA MPANGO WA KUSAIDIA MAWASILIANO KATIKA HALMASHAURI ELGA

 Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
HALMASHAURI ya Wilaya ya Mkuranga imekuja na mpango kabambe wa mfumo wa tehama ambao utaweza kusaidia mawasiliano kati ya Wananchi Wadau na Halmashauri zote nchini.

Hayo yameleezwa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Mhandisi Mshamu Munde alipokuwa akiwasilisha mpango huo kwa wajumbe wa Mkutano wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(ALAT) unaondelea jijini Dar es Salaam.
Munde amesema kuwa mfumo huo ambao unafahamika kama ELGA ambao unafanana kabisa na kama mfumo wa E.Gov ambapo mfumo huu utasaidia kufanya kazi kwa uraisi.

“sisi kama Halmashauri ya Mkuranga tunataka mfumo huu uweze kusambaa nchi nzima hili Halmashauri ziweze kufanya mawasiliano ya kibiashara kwa uraisi na kuwawezesha wananchi wake” amesema Mhandisi Munde

Munde ameongeza kuwa kama Halmashauri zote zitafanikiwa kutumia mfumo huu zitasaidia katika kuinua uchumi wa Viwanda kama anavyosema Mh Rais.
Anasema umefika wakati sasa kwa wakurugenzi wa Halmashauri zote kutumia mfumo huu hiliwaweze kusaidia kuinua uchumi wa Tanzania.
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, Mhandisi Mshamu Munde  akizungumza na wajumbe wa Mkutano wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(ALAT ) Juu ya mpango wa matumizi ya teknolojia ya huduma kwa njia ya mtandao ELGA.
 Wajumbe wa Mkutano wa 33 wa  Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Wajumbe wa Mkutano wa 33 wa  Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa uliofanyika jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad