Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
HALMASHAURI ya Wilaya ya Mkuranga imekuja na mpango kabambe wa mfumo wa tehama ambao
utaweza kusaidia mawasiliano kati ya Wananchi Wadau na Halmashauri zote nchini.
Hayo yameleezwa
na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Mhandisi Mshamu Munde alipokuwa akiwasilisha
mpango huo kwa wajumbe wa Mkutano wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa(ALAT) unaondelea jijini Dar es Salaam.
Munde
amesema kuwa mfumo huo ambao unafahamika kama ELGA ambao unafanana kabisa na
kama mfumo wa E.Gov ambapo mfumo huu utasaidia kufanya kazi kwa uraisi.
“sisi kama
Halmashauri ya Mkuranga tunataka mfumo huu uweze kusambaa nchi nzima hili
Halmashauri ziweze kufanya mawasiliano ya kibiashara kwa uraisi na kuwawezesha
wananchi wake” amesema Mhandisi Munde
Munde
ameongeza kuwa kama Halmashauri zote zitafanikiwa kutumia mfumo huu zitasaidia
katika kuinua uchumi wa Viwanda kama anavyosema Mh Rais.
Anasema umefika
wakati sasa kwa wakurugenzi wa Halmashauri zote kutumia mfumo huu hiliwaweze
kusaidia kuinua uchumi wa Tanzania.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, Mhandisi Mshamu Munde akizungumza na wajumbe wa Mkutano wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(ALAT ) Juu ya mpango wa matumizi ya teknolojia ya huduma kwa njia ya mtandao ELGA.
Wajumbe wa Mkutano wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Wajumbe wa Mkutano wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa uliofanyika jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment