HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 4, 2017

BENKI YA UBA TANZANIA WAZIDI KUNG'ARA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA

 Afisa huduma kwa wateja wa Benki ya UBA Tanzania, Bi Stella Matau akifurahia kumuhudumia mmoja wa wateja wao wakubwa aliyefika katika benki hio huku benki hio ikiendelea kung'ara katika kutoa huduma bora kwa wateja kwa wakati wote
Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya UBA Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wateja wao waliofika katika benki hio kwaajili ya kupata huduma za kibenki
Meneja Uendeshaji wa Benki ya UBA Tanzania, Bw Chriss Byaruhanga (wa Kwanza kushoto) akikata keko na baadhi ya wateja wao ikiwa ni ishara ya kuendeleza shamrashamra za wiki ya huduma kwa wateja ambapo wateja hao wameisifu benki hio kwa kutoa huduma bora wakati na sio kwa kipindi cha kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja.
Meneja Uendeshaji wa Benki ya UBA Tanzania, Bw Chriss Byaruhanga akigawa keki kwa baadhi ya wateja na wafanyakazi wa benki hio ikiwa ni ishara ya kuzindua wiki ya huduma kwa wateja.
Mmoja wa wateja wa benki ya UBA Tanzania akipata huduma ya kuweka pesa 
Mkuu wa idara ya masoko wa benki ya UBA Tanzania, Brendasia Kileo akigawa keko kwa mmoja wa wateja waliokuwa wakipata huduma ndani ya benki mapema leo ikiwa ni muendelezo wa wiki ya Huduma kwa wateja
Wiki ya huduma kwa wateja inaendelea huku benki ya uba tanzania ikiendelea kutoa huduma bora na zenye kutimiza malengo ya wateja wao huku kituo chao cha huduma kwa wateja kikiendelea kushika hatamu kwa wateja wao kwa kuwapa huduma bora masaa 24. Uba Bank ambao hivi karibuni walijidhatiti tena kwa kuanzisha kituo cha huduma kwa wateja kwa masaa 24 wamezidi kuwapatia huduma bora wateja wao bila kuangalia kuwa ni wiki ya huduma kwa wateja wao Hutoa huduma bora siku zote.
Uba bank wanafurahi kuwahudumia wateja wao siku zote huku wiki ya huduma kwa wateja ikiendelea kuwa sehemu tu ya kuendeleza kutoa huduma bora kwa wateja.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad