HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, October 31, 2017

ATHMANI ANAWAOMBA MSAADA WATANZANIA

Na Yeremias  Ngerangera, Namtumbo

Athmani  Amani  mkazi wa kijiji  cha Naikesi  kata ya kitanda  wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma  anawaomba  watanzania  kumsaidia  fedha  za kugharimia  matibabu  ya mtoto  wake  Shaziri  Athmani (12) anayesumbuliwa  na tatizo  la moyo kuwa  mkubwa.
Mtoto  Shaziri  Athamani  ni mwanafunzi  wa darasa  la nne  shule  ya msingi Naikesi  iliyopo  kata ya Kitanda  wilayani Namtumbo  awali  alikuwa anasumbuliwa  na kuvimba  miguu  hali iliyokuwa  inamkosesha  masomo  yake  darasani  mara kwa  mara kuanzia  mwaka  2016.
Mwaka  huo  huo  mwezi  Septemba  baba yake  alilazimika kumpeleka  Hospitali  ya Mkoa  Songea  kuangalia tatizo  la kuvimba  kwa  miguu  ya mtoto huyo  na  baada ya kupata  vipimo  wakashauriwa  kuenda  Hospitali  ya  Peramiho  .
Bwana  Athamani  alidai  kuwa  hakuwa  na fedha  za kumpeleka  mtoto  peramiho  kwa  kipindi  hicho  na badala yake  alirudi  naye  nyumbani  Naikesi  kwenda  kuuza  mifugo  lakini fedha hizo  hazikumwezesha  kukidhi  mahitaji  ya  kumtibu  mwanoa katika  Hospitali  ya  Peramiho  baada  ya  kufika  katika  Hospitali  hiyo  na kumaliza  fedha  yake  yote  aliyokuwa  nayo  katika  vipimo  pekee .
Baada  ya kupatiwa  vipimo  na  kubaini  Tatizo la  mwanae  alirudi  na mwanae  mpaka  kijijini  kwake  kujipanga  upya  kwa  ajili  ya  matibabu ya  mwanae  na  kujitahidi  kwa kile  anachokipata  anunue  dawa  kwa  ajili  ya  mwanae  huyo.
Pamoja  na  jitihada  hizo  hali ikaendelea kuwa  sio  nzuri  na ndipo  alipolazimika kufanya  kazi  za  kulima  mashamba  ya watu  ili apate  fedha  za kumtibu  kijana wake  na  mwaka  huu  mwezi  oktoba  alimpeleka  kijana wake  huyo  peramiho  na  baada  ya  kufika  peramiho  na kupatiwa  vipimo  alishauriwa  na  madaktari  kumpeleka  mtoto  huyo  Hospitali  ya  Muhimbili Dar es Salaam.
Hata  hivyo  mzazi  huyo  alifika  katika  ofisi  ya  Katibu  tawala  wa wilaya  ya  Namtuimbo  na kufanya  mazungumzo  na  Kaimu  katibu  tawala  wa wilaya  ya Namtumbo   Alkwin  Ndimbo  kwa  lengo  la  kupatiwa  msaada  wa matibabu  wa  kijana  wake  huyo.
Alkwin  alidai kuwa  kuna  sababu  ya  watanzania  wenye  moyo  kumsaidia  mtoto  huyo  kwa  michango  yao  ili  mzazi  wa kijana  huyo  aweze kumpeleka  kijana  wake  huyo  Hospitali ya Taifa  Muhimbili  na  bila  michango  kutoka  kwa  watanzania wenye  moyo  mzazi huyo  hana uwezo  wa  kumpeleka  kijana wake huyo  Hospitali  ya Taifa Muhimbili.
Kwa  watanzania  wenye  moyo  wa  kumsaidia  mtoto  huyo  wanaweza  kumpigia  mzazi wake  kupitia  namba  0629629872  au  unaweza  kumtumia  fedha  kupitia  namba  hiyo  ambapo  kwa  sasa  mzazi huyo  amerudi  kijijini  kwake  Naikesi  akiwa  na  mgonjwa  wake  akihangaika  kupata fedha  za  kumpeleka  mtoto wake huyo  Hospitali  ya Taifa  Muhimbili.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad