HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, October 23, 2017

AIRTEL TIMIZA VIKOBA SULUHISHO TOSHA VIKUNDI VYA AKINAMAMA

Mkuu wa kitengo cha Masoko na Airtel Money Bw, Isack Nchunda akiongelea mafanikio na mikakati yao katika kuikuza na kuieneza huduma ya ‘Airtel Money Timiza vikoba’ jinsi inavyotoa suluhisho kwa akinamama na vikundi mbalimbali vya Vikoba nchini.

Huduma ya Airtel Timiza vikoba imeendelea kuwa suluhisho tosha kwa makundi ambayo yanataka kuweka akiba na kujipatia mikopo ili kuendesha biashara zao vizuri.

Makundi mengi ya Vikoba sasa hivi yameamua kutumia huduma ya Airtel Timiza Vikoba kwani imewasaidia kuweka utaratibu mzuri huku serikali ikitaka vikundi vya vikoba visambae zaidi nchini ili watu wengi waweze kufaidika.

Hivi karibuni akizindua mradi wa vikoba katika eneo la Bunju Jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi aliwataka viongozi wa vikoba kuhaikisha wanatanua mitandao yao ili wananchi wengi zaidi wafaidi.

“Natoa wito kwa viongozi wa Vikoba kuhakikisha wanatanua mtandao wao wa vikoba nchinzima ili watu wengi zaidi waweze kufaidi,” aisema Mkuu wa Wilaya.

Airtel Timiza Vikoba imekuwa gumzo kubwa sasa hivi hasa baada ya kampuni ya Airtel kushirikiana na Benki ya Maendeleo kuhakikisha Vikoba vinakuwa rasmi zaidi na vinafanya shughuli zake kwa umakini zaidi tofauti na hapo mwanzo.

“Hadi sasa tangu mradi huu uanze imeshatolewa mikopo 487 yenye thamani ya Tsh milioni 20.5 kwa wanachama wa vikoba,” alisema Ibrahim Mwangalaba ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo.

Alisema jumla ya wateja 5,685 wameshajiunga na mfumo huu na kuunda makundi huku akaunti mpya 1,1810 zikifunguliwa. Alitoa wito kwa wanachama zaidi kujiunga na mfumo huo kwani ndio imekuwa suluhisho tosha kwa matatizo yanayokumba vikundi vingi vya vikoba.

Tangu mradi huu uzinduliwe, makundi 18,166 yenye wanachama 178, 638 yameshasajiliwa Mwangalaba aliongeza.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Masoko na huduma ya Airtel Money wa Airtel Tanzania Isack Nchunda alisema wanajivunia kwa kuweza kuleta suluhisho na sasa hivi wamelenga kuhakikisha malengo ya serkali ya kuhakikisha kunakuwepo na vikoba nchi nzima yanatimia kikamilifu.

“Makundi mengi ya vikoba yalikuwa yanapata shida hasa katika kuweka kumbukumbu na wakati mwingine vitabu vyao hupotea hivi kuwafanya washindwe kuwa na kumbukumbu sahihi. Wengine walikuwa wanatunza fedha kwenye vibubu, chini ya magodoro lakini huduma hii itawasaidia kuweka akiba zao vizuri kupitia Airtel Money ambapo wanachama wote wanaweza kufuatilia,” alisema huku akiongeza kuwa mwenyekiti tu ndiye mwenye mamlaka ya kuwa na nywila wanachama wanatumiwa ripoti tu.

Alisema huduma hii pia imesaidia kuimarisha uwazi katika makundi ya vikoba na Airtel itaendelea kufungua milango zaidi ili kuhakikisha watu wengi zaidi hasa wafanyabiashara wadogo wanapata huduma sahihi za kifedha.

Airtel Timiza Vikoba ilizinduliwa miezi mitano iliyopita ikiwa na lengo la kusaidia makundi mbalimbali kufikia malengo yao.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad