Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akitoa hotuba wakati wa uzinduzi wa Bodi mpya Kituo cha Uwekezaji (TIC )na tovuti ya jijini Dar es Salaam leo.
Akizungumza katika uzinduzi wa Bodi hiyo Mwijage amesema kuwa "Tunapambana kuondoa urasimu,tayari tumeanzisha kamati ya kitaifa ya kuhudumia wawekezaji na wajumbe ni taasisi zote zinazotoa huduma kwa wawekezaji, Mpaka sasa matokeo ni mazuri na tumeanza kupata ripoti za kutupongeza katika juhudi zetu za kuondoa urasimu kwenye utoaji wa vibali na leseni mbalimbalihapa nchini"
Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo cha Uwekezaji (TIC),Profesa Longinus Rutasitara Bodi akizungumza wakati wa uzinduzi wa Bodi mpya na tivuti ya TIC jijini Dar es Salaam leo. Amesema kuwa Bodi yetu itatoa ushirikiano kuhakikisha majukumu ya TIC yanatimizwa ipasavyo.
Tunapambana kuondoa urasimu, tayari tumeanzisha kamati ya kitaifa ya kuhudumia wawekezaji na wajumbe ni taasisi zote zinazotoa huduma kwa wawekezaji. Mpaka sasa matokeo ni mazuri na tumeanza kupata ripoti za kutupongeza katika juhudi zetu za kuondoa urasimu kwenye utoaji wa vibali na leseni mbalimbali.
No comments:
Post a Comment