HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 22, 2017

WAZIRI KAIRUKI AZINDUA BODI YA PILI YA UONGOZI INSTITUTE

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki amesema kuwa wakurugenzi walioteuliwa katika bodi ya Taasisi ya Uongozi  ni watu makini na wenye uzoefu wa muda mrefu katika nafasi mbalimbali hivyo watatoa ushauri mzuri kwenye taasisi hiyo.

Waziri Angellah aliyasema hayo katika uzinduzi wa bodi ya pili ya Taasisi  ya Uongozi uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini  Dar es Salaam. Amesema bodi ya wakurugenzi wa taasisi hiyo wamepita katika utumishi na wazalendo katika sehemu zao mbalimbali ambapo watakuwa msaada mkubwa kwa taasisi hiyo katika  kutoa ushauri.

Amesema kuwa Uongozi Institute ilianzishwa kwa ajili ya kuwajengea uwezo viongozi wa Afrika katika kuangalia maendeleo endelevu ya bara la Afrika  hivyo wajumbe wa bodi ni wa kimataifa na wanatambulika.

Angellah amesema kuwa walioteuliwa na Rais Dk.John Pombe Magufuli watatimiza majukumu yao na wataendelea kupewa ushirikiano pamoja na viongozi wengine wa Afrika katika kuwa na ajenda ya kuandaa viongozi.

Amesema uongozi Institute inatakiwa kutimiza mambo matatu moja ni bidhaa ya huduma iliyo na kiwango bora, kuangalia rasilimali  ya kuweza  kufanya taasisi hiyo ikue katika kuangalia vyanzo vya mapato pamoja na kujengea uwezo wa kuendelea kutekeleza ajenda ambazo zimeibuliwa.

Walioteuliwa katika bodi hiyo Mwenyekiti ni Balozi wa Finland Inchini Afrika Kusini, Kari Alanko , Makamu wa Rais Profesa Idris Kikula wengine ni Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora  Dk. Laureane Ndumbaro,  Katibu Mtendaji wa SADC Dk. Stergomena Tax, Profesa Penina Mlama wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Christina Duarte Waziri wa Zamani wa Fedha , Mipango na Utumishi wa Cape Verde, Mkurugenzi wa Nodic Afrika ya nchini Sweeden Lina Soiri, pamoja Mkurugenzi wa zamani wa shule ya utawala ya nchini Uingereza , David Walker.

Nae Afisa Afisa Mtendaji Mkuu wa Uongozi Institute, Profesa Joseph Semboja  amesema kuwa chombo hicho kilianzishwa katika kuwajengea viongozi wa Afrika ambao waliridhia kuundwa kwa chombo hicho.

Amesema kuwa Taasisi hiyo imetoa mafunzo mbalimbali tangu kuanzishwa kwake na itaendelea kutoa mafunzo kwa watumishi.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki akizungumza katika uzinduzi wa bodi ya pili ya Wakurugenzi wa Uongozi Institute , uliofanyika katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Uongozi Insitute, Profesa Joseph Semboja akizungumza katika uzinduzi wa bodi ya Uongozi Institute  juu ya taasisi hiyo inavyofanya kazi  katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Uongozi Institute ,Balozi wa Finland Inchini Afrika Kusini, Kari Alanko akitoa shukurani kwa Waziri Kairuki  mara baada ya kuzinduliwa  bodi hiyo.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki akigawa vitabu vya miongozo kwa wajumbe wa Bodi hiyo.
 Sehemu watendaji mbalimbali wa serikali waliohudhuria uzinduzi wa bodi ya pili ya oungozi institute.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki akiwa katika picha ya pamoja na bodi ya ya wakurugenzi ya Uongozi Institute, jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad