HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 22, 2017

TIMU YA NDANTO FC YATWAA KOMBE LA MICHUANO YA 'TULIA CUP 2017'

Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Davis Mwamunyange, akimkabidhi Kombe Nahodha wa timu ya Ndanto Fc, Peter Mwakingwa, baada ya kushika nafasi ya nafasi ya kwanza na kutwaa kombe la fainali za 'Tulia Cup 2017' kwenye uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya. Picha na Muhidin Sufiani (MAFOTO MEDIA GROUP)
Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Davis Mwamunyange, akimkabidhi Kombe Nahodha wa timu ya Isange, Frank Asilih, baada ya kushika nafasi ya pili katika fainali za 'Tulia Cup'kwenye uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya.
Beki wa timu ya Isange Fc, Zawadi Andombwisye (kushoto) akichuana kuwania mpira na mshambuliaji wa Ndanto Fc, Erick Mwangoye, wakati wa mchezo wa Fainali za 'Tulia Cup' uliochezwa jana Sept 21, 2017 kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya. Katika mchezo huo Ndanto walishinda kwa mabao 2-1 na kutwaa kombe hilo kwa mwaka huu 2017 na kitita cha sh. milioni 1.5.
Beki wa timu ya Ndanto Fc,Fidelis Yeo (kulia) akiwania mpira na mshambuliaji wa Isange Fc, Hussein Thom, wakati wa mchezo wa Fainali za 'Tulia Cup' uliochezwa jana Sept 21, 2017 kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya. Katika mchezo huo Ndanto walishinda kwa mabao 2-1 na kutwaa kombe hilo kwa mwaka huu 2017 na kitita cha sh. milioni 1.5.
Wachezaji wa Isange Fc, Shadrack Kandrum (kushoto) na Hussein Thom (kulia) wakimdhibiti Mandela Chaile, wakati wa mchezo wa Fainali za 'Tulia Cup' uliochezwa jana Sept 21, 2017 kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya. Katika mchezo huo Ndanto walishinda kwa mabao 2-1 na kutwaa kombe hilo kwa mwaka huu 2017 na kitita cha sh. milioni 1.5. 
Beki wa timu ya Isange Fc, Shadrack Kandrum (kulia) akimdhibiti mshambuliaji wa Ndanto Fc, Julius Mtawala, wakati wa mchezo wa Fainali za 'Tulia Cup' uliochezwa jana Sept 21, 2017 kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya. Katika mchezo huo Ndanto walishinda kwa mabao 2-1 na kutwaa kombe hilo kwa mwaka huu 2017 na kitita cha sh. milioni 1.5.
Luteni General, James Mwakibolwa, akiongozana na Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Tulia Ackson, kukagua timu ya Ndanto fc kabla ya mchezo wa fainali dhidi ya Isande Fc, katika mchezo wa fainali wa 'Tulia Cup' kwenye uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya.



Luteni General, James Mwakibolwa, akimkabidhi Kombe Nahodha wa timu ya Netiboli ya Kimo,Salome Sanyondo, baada ya kushika nafasi ya pili katika fainali za 'Tulia Cup'kwenye uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya. 

Luteni General, James Mwakibolwa, akimkabidhi Kombe Nahodha wa timu ya Netiboli ya Wizara ya Mambo ya Ndani, baada ya kushika nafasi ya kwanza katika fainali za 'Tulia Cup'kwenye uwanja wa Tandale Tukuyu Wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad