Mkurugenzi wa Maendeleo ya Viwango wa Shirika la Viwango
Tanzania (TBS), Bi. Edna Ndumbaro akisisitiza jambo kwenye Semina ya
wadau kwenye semina iliyowakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo
wahandisi, makandarasi, wazalishaji, wasambazaji na watumiaji wa nyaya
za umeme jijini Dar es Salaam jana kuhusu matumizi ya Rangi mpya za
nyaya za umeme.
Afisa Viwango wa Viwango wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS),
Bw. Henry Massawe akiwasilisha mad kwenye Semina ya wadau kwenye
semina iliyowakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo wahandisi,
makandarasi, wazalishaji, wasambazaji na watumiaji wa nyaya za umeme
jijini Dar es Salaam jana kuhusu matumizi ya Rangi mpya za nyaya za
umeme.
Baadhi ya washiriki wa semina ya wadau kwenye semina
iliyowakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo wahandisi, makandarasi,
wazalishaji, wasambazaji na watumiaji wa nyaya za umeme jijini Dar es
Salaam jana kuhusu matumizi ya Rangi mpya za nyaya za umeme semina
hiyo imeandaliwa na Shirika Viwango wa Shirika la Viwango Tanzania
(TBS).
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
WADAU katika sekta ujenzi nchini wametakiwa kutumia bidhaa zenye
viwango na ubora unaostahili ili kulinda ukuaji wa sekta hiyo na
kuleta matokea chanya kwa ustawi na maendelea ya taifa na watu wake.
Akizungumza kwenye semina iliyowakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo
wahandisi, makandarasi, wazalishaji, wasambazaji na watumiaji wa nyaya
za umeme jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Viwango
wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Bi. Edna Ndumbaro alisema
bidhaa zinazotumika kwenye masuala ya umeme zinahitaji kuwa na
viwango na ubora unaostahili.
“Badiliko la rangi mpya za nyaya za umeme (New Colour Codes)
limewaleta wadau hawa muhimu kujadiliana kwa pamoja na kuazimia kwa
pamoja namna bora ya utekelezaji wake,” Bi. Ndumbaro alisema.
Alisema rangi mpya ya nyaya ya umeme ilishaazimiwa kama kiwango cha
lazima kufuatwa tangu mwaka 2016 na hivyo ni vyema kwa wadau na
wataalamu wakazingatia kuwa viwango ni jambo muhimu sana likapewa
kipaumbele zaidi.
“Sisi kama TBS tutaendelea kutoa elimu juu ya umuhimu wa viwango na
ubora kupitia vyombo mbalimbali vya habari na mitandao ya kijamii
ikiwemo tovuti ya shirika,” Bi. Ndumbaro alisema na kuongeza kuwa
washiriki wa semina hiyo watakuwa walimu wazuri.
Awali, Afisa Viwango wa TBS, Bw. Henry Massawe katika Mada yake
aliyoiwasilisha katika semina hiyo, alisema rangi mpya za nyaya za
umeme zitasaidia kuzuia uwezekano wa kuyumbisha bei za nyaya ya umeme.
Bw. Massawe ambaye aliwasilisha mada kuhusu mahitaji ya utambuzi wa
viwango na rangi za nyaya za Umeme alisema ni vizuri wadau wakatambua
kuwa Viwango vifuatwe kabla ya matumizi.
“Viwango vikifuatwa na kuzingatiwa katika matumizi ya vifaa ya nyaya
za umeme vitapunguza kama siyo kuondoa kabisa madhara ya vifaa umeme
vinavyoingizwa kutoka nje,” Bw. Massawe alisisitiza.
Kwa upande wake, Mshiriki kutoka Kampuni ya NAMIS Corporate Limited,
Bwana Bright Naimani alisema badiliko la Rangi mpya za nyaya za umeme
ni muhimu katika kulinda ubora na kiwango kwani wadau walipata fursa
ya kujifunza na kujadiliana masuala mbalimbali ya viwango.
Semina hiyo ambayo iliandaliwa na TBS kwa lengo la kuhamasisha na
kuwajengea uwezo wadau mbalimbali umuhimu wa matumizi ya rangi mpya
za nyaya za umeme.
No comments:
Post a Comment