HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 22, 2017

SHEIKH HAMID JONGO AWATAKA WANAFUNZI NA WALIMU WA SHULE YA VUCHAMA KUJIPANGA KATIKA USHINDANI WA KITAALUMA

Mjumbe wa baraza la Ulamaa BAKWATA taifa, ambaye pia ni Imamu Mkuu wa Msikiti wa Manyema jijini Dar es salaam, Sheikh Hamid Jongo akizungumza na wanafunzi, walimu na wazazi wa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Vuchama iliyopo Ugweno, Mwanga Mkoani Kilimanjaro, katika mahafali ya kuwaaga wanafunzi wa kidato cha nne.
Meneja wa shule ya sekondari ya Vuchama, Alhaj Yusuph Mfinanga, akizungumza na wanafunzi, walimu na wazazi wa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Vuchama iliyopo Ugweno, Mwanga Mkoani Kilimanjaro.
Mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Vuchama, Mwalimu Juma A. Juma akizungumza na wanafunzi, walimu na wazazi wa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Vuchama iliyopo Ugweno, Mwanga Mkoani Kilimanjaro,katika mahafali ya kuwaaga wanafunzi wa kidato cha nne.

Na Mwamvua Mwinyi, Kilimanjaro

MJUMBE wa baraza la Ulamaa(BAKWATA)Taifa,ambae pia ni Imamu mkuu wa msikiti wa Manyema jijini Dar es salaam, Sheikh Hamid Jongo, amewataka wanafunzi wa shule za taasisi za kielimu za kidini kusoma kwa bidii na kuwa watiifu badala ya kuwa wajeuri na mafedhuri.

Ameeleza watoto wanapaswa kujipanga kitaaluma ya ahera na kidunia ili kukua katika misingi iliyo na maadili mema ya kidini na kitaifa. Aidha sheikh Jongo,ameziasa taasisi hizo waache kufundisha uhasi bali zijiongeze,kubuni mbinu mbadala zitakazowezesha kwenda pamoja na ushindani wa kitaaluma kwa lengo la kufaulisha hasa kidato cha nne na cha sita pasipo kushika mkia.

Aliyaelezea hayo, wakati akizungumza na wanafunzi, walimu na wazazi katika shule ya kiislamu ya sekondari ya VUCHAMA ,iliyopo Ugweno,wilaya ya Mwanga, Kilimanjaro,kwenye mahafali ya kuwaaga wanafunzi wa kidato cha nne. Sheikh Jongo,alisema elimu ni silaha ya maisha na msingi wa kimaendeleo hivyo ,wanafunzi hao wajitahidi kuondokana na ujinga kwa manufaa yao ya baadae .
Alifafanua kwamba,walimu wa shule hizo wawafundishe wanafunzi wao utiiifu ili kuishi vizuri na kuwa wazalendo na nchi yao.

“Ikiwa tunapita mashuleni na kuwasomesha masomo ya dini na miongoni wa maeneo tunayowapa yakiwa ni ya uhasi hilo ni suala baya sana, kitawagharimu waislamu kweli, kwani matokeo yake kuna vijana wamekuwa wajeuri ,mafedhuri hata kwa mashehe zao”

“Kijana wa aina hiyo mnatarajia awe kiongozi wa baadae wa kiroho kwelii?hawa ndio wanaohangaisha hata nchi,hivyo ,walimu tujitahidi kufundisha maadili mema ya kidini na kimaisha kijumla”alisema sheikh Jongo.

Hata hivyo Sheikh Jongo ,aliwaomba waislamu wamuogope mwenyezi mungu,waendelee kukubaliana na imani ya kiislamu na kuwaomba baadhi yao kuacha fikra potofu ya imani za itikadi za kisiasa ama siasa kali. Alibainisha,watu wenye itikadi kali hata mtume S.A.W hajawahi kukubaliana nao katika enzi hizo,hivyo kumcha mungu ukiwa na siasa kali utakuwa na kasoro.
Sheikh huyo,alitoa rai kwa watanzania kijumla kuishi kwa amani na utulivu ili kuendelea kujenga heshima ya taifa. Wakati huo huo meneja wa shule ya kiislamu ya sekondari ya Vuchama,alhaj Yusuph Mfinanga,aliwasihi wahitimu wa kidato cha nne shuleni hapo kwenda kuyaendeleza mazuri na heshima waliyoipata wakiwa shule.

Alisema shule hiyo ina chumba cha kufundishia TEHAMA chenye computer 30 itakayowasaidia watoto kuondoka wakiwa na uelewa juu ya masuala ya mitandao,chumba cha maabara ya masomo ya sayansi na maktaba. Alhaj Mfinanga alitoa ofa kwa mwanafunzi atakaefaulu na amekuwa akitoa motisha mbalimbali kwa walimu .

Alisema kwasasa wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa msikiti ambapo kwasasa wanasalia ndani ya madarasa ,:”Inatakiwa sh.mil.105 ili kukamilihsa msikiti wanaotarajia kuanza kuujenga. Nae mkuu wa shule ya kiislamu ya sekondari ya Vuchama,Juma .A.Juma,aliishauri serikali kuiangalie kuwapelekea mafungu ya wilaya ya kuendeleza shule kama zimefanya vizuri.
Alisema shule za binafsi zimekuwa ni moja ya shule zinazofanya vizuri lakini zimekuwa hazipewi mafungu hayo hali ambayo imemsukuma aombe wizara ya elimu kuliona hilo. Shule ya kiislamu ya sekondari ya Vuchama,imesajiliwa mwaka 2014,kwa wanafunzi wa kidato cha I hadi IV. Ilianza rasmi mwaka 2015 ikiwa na wanafunzi wawili na sasa ina wanafunzi 267 kati yao wanaohohitimu kidato cha nne ni 33.

Shule ya Vuchama ni moja ya shule zinazomilikiwa na mfanyabiashara Yusuph Mfinanga,ambapo ana chuo cha masuala ya utalii Njuweni Institute,hotel ya Njuweni na shule ya msingi Kibaha Independent-KIPS zilizopo Kibaha mkoani Pwani .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad