Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo (kushoto) na Brigedia Jenerali Dkt. Paul Massawe wakiangalia majeraha aliyopata Meja Jenerali Mstaafu Vicent Mritaba baada ya kushambuliwa kwa risasi mkononi, tumboni na kiunoni wakati anaingia nyumbani kwake Ununio wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 12 Septemba, 2017 ametembelea hospitali ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Lugalo, Jijini Dar es Salaam na kumjulia hali Meja Jen. Mstaafu Vincent Mribata aliyelazwa hospitalini hapo baada ya kushambuliwa na watu wenye silaha wakati akiingia nyumbani kwake Ununio, Kinondoni Jijini Dar es Salaam.
Meja
Jen. Mstaafu Mritaba alishambuliwa kwa risasi jana tarehe 11 Septemba, 2017
majira ya mchana na kisha kukimbizwa katika hospitali ya Jeshi Lugalo kwa
matibabu.
Mkuu
wa kituo cha tiba cha hospitali hiyo na daktari bingwa wa magonjwa ya moyo
Brigedia Jenerali Paul Massawe amemueleza Mhe. Rais Magufuli kuwa Meja Jen.
Mstaafu Vincent Mritaba anaendelea vizuri baada ya madaktari kufanikiwa kutoa
risasi alizopigwa mkononi, kiunoni na tumboni.
Meja
Jen. Mstaafu Mritaba amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kumjulia hali na kumuombea dua ili apone haraka.
Mhe.
Rais Magufuli aliyeongozana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jen. Venance Mabeyo
pia ametembelea wodi ya majeruhi na kuwajulia hali wagonjwa wanaotibiwa katika
wodi hiyo na baadaye akawasalimu wananchi waliofika hospitali hapo kwa ajili ya
kupata matibabu.
Mhe.
Dkt. Magufuli amewapongeza Madaktari wa hospitali ya Jeshi Lugalo kwa huduma za
matibabu wanazotoa kwa askari na wananchi wengine na amewahakikishia
kuwa Serikali itaendelea kufanyia kazi changamoto mbalimbali zinazowakabili
katika utekelezaji wa majukumu yao.
ais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo (kushoto) wakioneshwa na Brigedia Jenerali Dkt. Paul Massawe Brigedia baadhi ya risasi zilizotolewa kwenye mwili wa Meja Jenerali Mstaafu Vicent Mritaba baada ya kushambuliwa wakati akiingia nyumbani kwake Ununio wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo (kushoto) na Brigedia Jenerali Dkt. Paul Massawe, Brigedia Jenerali Mstaafu Vicent Mritaba na wauguzi wakiomba dua wakiongozwa na Mama Margareth Vicent Mritaba hospitali ya Jeshi Lugalo jijini Dar es salaam alikolazwa Meja Jenerali Mritaba akitibiwa majeraha baada ya kushambuliwa kwa risasi mkononi, tumboni na kiunoni wakati anaingia nyumbani kwake Ununio wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na mtoto Nathan Martin wakati akitoka kumjulia hali Meja jenerali Mstaafu Vicent Mritaba aliyelazwa Hospitali ya Jeshi Lugalo jijini Dar es salaam alikolazwa akitibiwa majeraha baada ya kushambuliwa kwa risasi mkononi, tumboni na kiunoni wakati anaingia nyumbani kwake Ununio wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwalimu Aloys Konolipa wa Shule ya Msingi Kidugalo wilayani Kisarawe Mkoa wa Pwani alipopita kuwapa pole wagonjwa wengine baada ya kumjulia hali Meja Jenerali Mstaafu Vicent Mritaba aliyelazwa Hospitali ya Jeshi Lugalo jijini Dar es salaam alikolazwa akitibiwa majeraha baada ya kushambuliwa kwa risasi mkononi, tumboni na kiunoni wakati akiingia nyumbani kwake Ununio wilaya ya Kinondoni. Picha na IKULU
No comments:
Post a Comment