HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 21, 2017

NAIBU SPIKA TULIA ACKSON AZINDUA JENGO LA MALIWATO YA WANAWAKE HOSPITALI YA WILAYA YA RUNGWE

Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tukuyu, Ezekiel Manyemele, wakifunua kitambaa kuzindua Jengo la Choo cha wanawake katika Hospitali ya Makandana Wilayani Rungwe, jana Sept 20, 2017. Jengo hilo la Choo limegharimu zaidi ya Sh. milioni 50.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, akipanda mti na Mwanafunzi wa darasa la Sita wa Shule ya Msingi Segera, Tunza Fred, wakati alipotembelea shule hiyo kukabidhi Vifaa vya ukarabati wa shule hiyo akiwa katika ziara yake Wilaya ya Rungwe jana Sept 20, 2017. Jumla ya miti 160 ilipandwa katika shule hiyo ikiwa ni sehemu ya kutunza mazingira.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, akimkabidhi tofali, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Segera, Fred Mfwea (wa pili kulia) na Diwani wa Kata ya Segera (katikati) wakati alipotembelea shuleni hapo kukabidhi Vifaa vya ukarabati wa shule hiyo akiwa katika ziara yake Wilaya ya Rungwe jana Sept 20, 2017.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, akicheza muziki 'Ndiyo Maana Tenzele' wa asili wa kabila la Wasafa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Unyamwange, Julius Pascal, wakati alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya akiangalisha fedha kwa ajili ya Ujenzi wa Kituo cha afya Kata ya Isongole jana sept 20,2017. tofali.Picha na Muhidin Sufiani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad