HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, September 23, 2017

MKUU WA MKOA WA TANGA APOKEA VIFAA TIBA KUTOKA KWA UZALENDO KWANZA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Martine Shigella, akitokea msaada wa vifaa tiba kutoka kwa Mwenyekiti wa UZALENDO KWANZA, Steve Nyerere wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa tiba iliyofanyika katika viwanja vya Tanga Manno mjini Tanga. PICHA ZOTE NA KAJUNASON/MMG - TANGA. 

 Vifaa vilivyotolewa na wasanii na wachezaji hao katika uwanja wa Tangamano ikiwa ni Kampeni ya Uzalendo kwanza ni pamoja na Ultra Sound, mashine ya X- Ray, Wheel Chair, Magongo ya walemavu na craches. 

 Shigella amepokea vifaa hivyo ikiwa ni moja ya Kampeni ya UZALENDO KWANZA ambayo inaongozwa na wasanii na wacheza mpira ikiwa na lengo la kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika kuchangia maendeleo ya nchi. Ambapo vifaa hivyo vinagawiwa katika hospitali za Ngamiani, Makorola, Pongwe na Mikanjuni.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Martine Shigella, akitokea msaada wa vifaa tiba kutoka kwa Mwenyekiti wa UZALENDO KWANZA, Steve Nyerere wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa tiba iliyofanyika katika viwanja vya Tanga Manno mjini Tanga.
Vijana wazalendo wa UZALENDO KWANZA wakibeba vifaa Tiba ambavyo walitoa kwa ajili ya hospitali za mkoa wa Tanga.
Mkuu wa mkoa wa Tanga, Martin Shigella aliwataka wasanii na wacheza mpira hao kuhakikisha wanatumia umaarufu walionao ili kuweza kuwavutia wawekazaji kutoka nje ya nchi ili kukuza uchumi wa nchi.

"Wasanii mnadhamana kubwa ya kuhakikisha mnatumia vema vipaji vyenu ili kuweza kusaidia juhudi kubwa zinazofanywa na serikali kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi ya viwanda kwa wao kuvutia wawekezaji ambao wanaweza kuwekeza katika nyanja mbalimbali." alisema 

 "Ninatambua asilimia kubwa mlizunguka kwenye kampeni mkiwaomba watanzania wamchague Rais Dkt. John Pombe Magufuli kutokana na dhamira yake nzuri ya kuletea maendeleo lakini pia hivi sasa mnashirikiana naye kwenye sekta ya afya kwa kumuunga mkono kwa kutoa mchango wenu niwaambie huu ni uzalendo ambao ni msingi wa maendeleo ya Taifa" 

 "Kwa mfano Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na wazee wengine walipigania Taifa hii kwa sababu ya uzalendo na ndio maana mnaona Rais wetu namna anavyopambana kuhakikisha rasilimali za Taifa zinalindwa na kutunzwa kwa ajili ya vizazi vya sasa na baadae kwa lengo la kila mtanzania kuweza kunufaika nazo "
Wananchi wakifuatilia wakati halfa ya ugawaji wa vifaa tiba. Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe, akiwashukuru UZALENDO KWANZA kwa jinsi walivyoweza kujitoa kwa hali na mali vifaa tiba kwa hospitali za mkoa wa Tanga.
Mkuu wa wilaya ya Tanga Mhe. Thobias Mwilapwa akitoa msisitizo kwa wasanii wa Tanga kuwa na moyo kama wa UZANDO KWANZA wa kuweza kujitoa kwa moyo mmoja wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa tiba iliyofanyika katika viwanja vya Tanga Manno mjini Tanga.
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga.Alhaji Mustapha Selebosi akitoa neno la shukrani wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa tiba iliyofanyika katika viwanja vya Tanga Manno mjini Tanga. 
Mwenyekiti wa UZALENDO KWANZA, Steve Nyerere akieleza machache wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa tiba iliyofanyika katika viwanja vya Tanga Manno mjini Tanga.

Akikabidhi vifaa hivyo, Mwenyekiti wa Kampeni ya UZALENDO KWANZA, Steven Mengele 'Nyerere' alisema uzalendo kwanza imemaua kuchangia vifaa tiba kwa hospitali ya Tanga na kwamba kampeni hizo zitaelekea mikoa mingine mbali mbali ikiwemo Lindi na Mtwara, Dodoma, Arusha, na Mwanza.
Mwenyekiti wa UZALENDO KWANZA, Steve Nyerere akiwatambulisha baadhi ya wazanii ambao wanaunda UZALENDO KWANZA.
Mkuu wa mkoa wa Tanga, Martin Shigella akimtunza msanii wa UZALENDO KWANZA ambaye alikuwa akitoa burudani.
Meza kuu ikifuatilia tukio wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa tiba iliyofanyika katika viwanja vya Tanga Manno mjini Tanga. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Martine Shigela, akifuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mjini, Mhe. Thobias Mwilapwa na mwenyekiti wa UZALENDO KWANZA, Steve Nyerere.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Martine Shigela, akiteta jambo na Mwenyekiti wa UZALENDO KWANZA, Steve Nyerere wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa tiba iliyofanyika katika viwanja vya Tanga Manno mjini Tanga. Kutoka kulia ni mkuu wa Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe, Mkuu wa wilaya ya Tanga Mhe. Thobias Mwilapwa na mwishoni kushoto ni Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga.Alhaji Mustapha Selebosi.
Wasanii wa UZALENDO KWANZA akitoa burudani wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa tiba iliyofanyika katika viwanja vya Tanga Manno mjini Tanga.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Martine Shigela, akisalimiana na Msanii Ruby ambaye ni mmoja ya wana UZALENDO KWANZA wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa tiba iliyofanyika katika viwanja vya Tanga Manno mjini Tanga. 
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Martine Shigela, akiteta jambo na Mwenyekiti wa UZALENDO KWANZA, Steve Nyerere.
UZALENDO KWANZA wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhi vifaa tiba.. Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigela akiwa ameongozana na Mkuu wa wilaya ya Tanga Mhe. Thobias Mwilapwa (wa kwanza kushoto), Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga.Alhaji Mustapha Selebosi (mwenye tisheti ya mistari) pamoja na Mwenyekiti wa UZALENDO KWANZA, Steve Nyerere  wakati akipokea vifaa tiba kutoka kwa UZALENDO KWANZA ambao wametoa vifaa tiba.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad