HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 27, 2017

CRDB BANK YAPIGA TAFU UKARABATI WA SHULE YA MSINGI GEZAULOLE

Katibu wa Benki ya CRDB na Mkurugenzi wa Maswala ya Kampuni, John Rugambo akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh. milioni mbili (2,000,000) kwa Wanafunzi, Kelvin James na Swaum Mohamed wa darasa la sita Shule ya Msingi Gezaulole, Kigamboni jijini Dar es salaam ikiwa ni mchango wa benki hiyo kusaidia ukarabati wa madarasa ya shule hiyo, leo Septemba 27, 2017.
 Katibu wa Benki ya CRDB na Mkurugenzi wa Maswala ya Kampuni, John Rugambo akizungumza kabla ya kabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh. milioni mbili (2,000,000) kwa ajili ya kusaidia ukarabati wa madarasa ya shule hiyo, leo Septemba 27, 2017. Kulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Mariam Kinande na kushoto ni Mwenyekiti aliyemaliza muda wake wa Kamati ya Shule ya Mshingi Gezaulole,Martin Madama.
 Katibu wa Benki ya CRDB na Mkurugenzi wa Maswala ya Kampuni, John Rugambo akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh. milioni mbili (2,000,000) kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Shule ya Mshingi Gezaulole, Bundala Maganga ikiwa ni mchango wa benki hiyo kusaidia ukarabati wa madarasa ya shule hiyo, leo Septemba 27, 2017. Wengine pichani ni Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Mariam Kinande (kulia) na kushoto ni Mwenyekiti aliyemaliza muda wake wa Kamati ya Shule ya Mshingi Gezaulole,Martin Madama.
Katibu wa Benki ya CRDB na Mkurugenzi wa Maswala ya Kampuni, John Rugambo akizungumza na baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Msingi Gezaulole, iliyopo Kigamboni jijini Dar es salaam.
Katibu wa Benki ya CRDB na Mkurugenzi wa Maswala ya Kampuni, John Rugambo  akiwa katika picha ya pamoja na Walimu na wanafunzi wa Shule ya Msingi Gezaulole, iliyopo Kigamboni jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad