HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, September 25, 2017

CRDB BANK YACHANGIA MIL. 100 ZA UJENZI WA OFISI ZA WALIMU JIJINI DAR

Mkurungenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 100 kwa ajili ya kusaidia Ujenzi wa ofisini za walimu wa Shule za msingi na Sekondari za jijini Dar es salaam, leo Septemba 25, 2017. Makabidhoano hayo yamefanyika kwenye ofisi ya ya Mkuu wa Mkoa. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa ofisi hizo za waalimu, Kanali Charles Mbuge na kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa kupokea mchango wa shilingi milioni 100 uliotolewa na Benki ya CRDB kwa ajili ya Ujenzi wa ofisi za waalimu jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurungenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei na kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa ofisi hizo za waalimu, Kanali Charles Mbuge.
Mkurungenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam wakati wa kukabidhi mchango wa shilingi milioni 100 uliotolewa kwa ajili ya Ujenzi wa ofisi za waalimu jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akifafanua jambo wakati akihamisha pesa kuchangia Ujenzi wa ofisi za walimu jijini Dar es Salaam kwa kutumia Huduma ya SimBanking, ambapo alichangia shilingi milioni moja.
Picha ya pamoja na kamati ya Ujenzi wa ofisi za walimu jijini Dar es Salaam. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad