Afisa habari baraza la sanaa Tanzania, Agness Kiwaga akizungumza na wasanii kuhusu elimu ya kujiunga na mfuko wa Pensheni wa PSPF, katika viwanja vya Basata leo Jijini Dar es Salaam.
Afisa masoko mfuko wa Pensheni wa PSPF, Magira Werema akizungumza na wasanii kwa ujumla kuhusu umuhimu wa kujiunga na mfuko wa Pensheni wa PSPF pamoja na faida watakazozipata kupitia mfuko huo leo katika viwanja vya Basata jijini Dar es Salaam.
Msanii mkongwe nchini Tanzania, Stara Thomas akizungumza na waandishi wa habari kuhusu walivyopokea wito huo na kutaka wasanii wenzake kuamka na kujiunga na mifuko ya Pensheni ili kuweza kupata mikopo mbalimbali, mafao ya uzeeni, mafao ya uzazi pamoja na fao la kifo.
Msanii Mkongwe Nkwama Badaga akizungumza na waandishi wa habari akiwataka wasanii wenzake kutumia fursa hiyo kujiunga na mfuko wa pesheni ili kujikwamua na maisha ya uzeeni na kusaidia familia.
Baadhi ya wasanii mbalimbali wakisiliza kwa makini elimu hiyo ya kujiunga na mfuko wa pensheni ili kunufaika na maisha ya sasa na baadae kipindi watakapochoka kufanya kazi za sanaa.
Meneja wa Bendi ya Msondongoma, Saidi Kibiriti akizungumza na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa BASATA jijini Dar es Salaam juu ya umuhimu wa kujiunga na Mfuko wa Pensheni wa PSPF kwaajili ya kuhifadhi na kutunza fedha kwa ajili ya kuwasaidia maisha ya baadae.
Na Agness Francis, Globu ya jamii.
MFUKO wa pensheni wa PSPF umewataka
wasanii wote nchini kujiunga na mfuko huo ili kurahisisha maisha na
kukidhi majanga yasiotarajiwa na bila
kujali wasanii walio popote nchini huduma hii kuwafikia.
hayo yamesemwa na Afisa Masoko wa mfuko wa PSPF, Magira Werema, wakati akizungumza na waandishi
wa habari Jijini Dar es Salaam leo, amesema kuwa licha ya kuwa wasanii hujipatia
vipato kutokana na kazi zao binafsi za ubunifu
upo umuhimu wa wasanii hao kujiunga na mfuko wa pensheni ili kuwasaidia kupata mafao ya uzeeni, Bima ya
afya na fao la kifo.
Nae afisa habari baraza la sanaa Tanzania (BASATA), Agness Kiwaga, amesema kuwa wasanii wajiunge kwenye
mfuko Mfuko wa Pensheni wa PSPF ili iwasaidie baade pale watakapo zeeka kwasababu uwezo wa
kufanya kazi zao utapungua hivyo basi
inakuwa ni rahisi kupata fao la uzeeni kwaajili ya kuasaidia familia zao.
Mwana muziki Mkongwe nchini, Stara Thomas, amesema kuwa imezoeleka vibaya kuwa sanaa sio kama kazi
zingine za taasisi kwa sasa ipo fursa
kwa wasaniii wenzake kujiunga na mfuko huo
ili kuweza kuwasaidia kupata mikopo mbalimbali.
Nae Msanii Nkwama Badanga, amesema kujiunga na mfuko huo wa pensheni itasaidia
kwa wasanii kujali na kujituma zaidi
kufanya kazi ili waweza kutimiza pesa ya mfuko ya kila mwezi ili kupata faida ya baadae na kuendelea
kusaidi familia kipindi watakapochoka kufanya kazi za sanaa.
Meneja wa bendi ya Msondongoma, Saidi Kibiriti amesema
kuwa wanamuziki wa zamani wa muziki wa dansi wengi wao wakishazeeka wanakuwa na hali ngumu ya kiuchumi mpaka
kufikia kuomba misaada hii hotokana na
kutokuwa na elimu kuhusu utunzaji wa
fedha kwa ajili ya maisha ya baadae ameona
umuhimui wa muamko kwa wanamuziki wenzake kujitokeza kupata elimu ya kujiunga na mifuko
ya pensheni nchini.
No comments:
Post a Comment