HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, August 16, 2017

Umoja wa Mataifa Wakataa Ombi la Raila Odinga

Afisa wa Umoja wa Mataifa, amekataa ombi la kiongozi wa Muungano wa Upinzani nchini Kenya Nasa, Raila Odinga la kutaka umoja huo kufanya tathmini mpya ya uchaguzi mkuu wa Agosti 8.

Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Farhan Haq, ameunga mkono kauli ya Katibu Mkuu, Antonio Gutrres, ya kuwataka wanasiasa wa Kenya wanaopinga matokeo ya uchaguzi kufikisha masuala hayo mbele ya taasisi zenye mamlaka ya kutoa maamuzi Kikatiba.

Bw. Haq amesema, Umoja huo utafuatilia kauli za Bw. Odinga kuhusu uchaguzi mkuu huku gazeti la Washington Post likisema uchaguzi wa Kenya ulikuwa huru na wa haki.

Chanzo: BBC Swahili

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad