Mkurugenzi Mtendaji wa NMB, Ineke Bussemaker, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Joyce Hagu, Mwenyekiti wa Bodi ya Nafasi Art Space, Davie Kitururu, Mkurugenzi wa Nafasi Art Space, Rebecca Correy na Balozi wa Denmark nchini, Einar Jensen wakifungua banda la NAFASI ya Watoto.
BENKI ya NMB Tanzania imedhamini ujenzi wa duka la Nafasi Art
litakalotumiwa na watoto kujifunza mambo mbalimbali ambayo yanahusu
sanaa ili kukuza vipaji walivyonavyo vya sanaa ili watakapokua waweze
kuvitumia kutengeneza kipato.
Akizungumza wakati wa hafla
ya ufunguzi wa duka hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa NMB, Ineke alisema
udhamini huo ni sehemu ya malengo ya benki kuhakikisha inatenga pesa
ambazo zitatumika kusaidia jamii.
"Benki yetu imekuwa
ikitumia kitengo cha CSR kusaidia jamii kwa kutenga pesa kila mwaka
ambazo zinatumika kusaidia jamii, tunaamini kuwa ujenzi huu utasaidia
kuinua vipaji vya watoto ambao wanapenda sanaa ili wainue vipaji vyao,"
alisema Ineke.
Naye Mkurugenzi wa Nafasi Art Space,
Rebecca Correy aliishukuru NMB kwa uufadhili ambao wamewapa na kuwa
banda hilo litawasaidia watoto wanaopenda sanaa kuonyesha vipaji vyao
kwani kwa kipindi kirefu watoto wamekuwa wakikosa nafasi ya kushiriki
kufanya kazi mbalimbali za sanaa lakini kwa sasa wataweza kuonyesha
vipaji vyao.
Kwa upande wa mgeni rasmi kwenye halfa hiyo,
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Joyce Hagu aliipongeza NAFASI Art
Space kwa jitihada ambazo inazifanya za kukuza sanaa nchini na kuwa
Serikali ya awamu ya tano itandelea kushirikiana nao.
Mgeni rasmi kwenye hafla ya uzinduzi wa banda la NAFASI ya watoto, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Joyce Hagu akikata utepe kufungua duka la kuhifadhia kumbukumbu la NAFASI Art Space. Mkurugenzi Mtendaji wa NMB, Ineke Bussemaker akizungumza kuhusu udhamini wa NMB na jinsi ambavyo wamejipanga kutoa misaada kwa jamii zenye uhitaji. Mkurugenzi wa Nafasi Art Space, Rebecca Correy akitoa neno la utangulizi. Mwenyekiti wa Bodi ya Nafasi Art Space, Davie Kitururu akitoa taarifa kuhusu taasisi hiyo. Balozi wa Denmark nchini, Einar Jensen akizungumza kuhusu Nafasi Art Space. Banda la NAFASI ya watoto. Banda la NAFASI ya watoto. Banda la NAFASI ya watoto.
Duka la kuhifadhia kumbukumbu la NAFASI Art Space. Duka la kuhifadhia kumbukumbu la NAFASI Art Space.
No comments:
Post a Comment