HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, August 15, 2017

Serikali yaipongeza Vodacom uorodheshwaji wa hisa DSE

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, (kulia)akipiga kengele kuashiria kuorodheshwa rasmi kwa hisa za kampuni ya Vodacom Tanzania PLC katika Soko la Hisa la Dar es Salaam jana. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Ian Ferrao na Afisa Mtendaji Mkuu wa DSE Moremi Marwa.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, (kulia) akimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao (katikati) kuhusiana na kufanikisha kuorodheshwa rasmi kwa hisa za kampuni yake katika Soko la Hisa la Dar es Salaam jana.Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa DSE Moremi Marwa.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, (wapili kulia) Mwenyekiti wa bodi ya soko la hisa, John Mduma (kulia) na Afisa Mtendaji Mkuu wa DSE Moremi Marwa wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC,Ian Ferrao akifafanua jambo wakati wa Uzinduzi wa hafla ya kuorodheshwa rasmi kwa hisa za kampuni ya Vodacom Tanzania PLC katika Soko la Hisa la Dar es Salaam jana.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, akiongea wakati wa  hafla ya  Uzinduzi wa kuorodheshwa rasmi kwa hisa za kampuni ya Vodacom Tanzania PLC katika Soko la Hisa la Dar es Salaam jana. Katikati ni Afisa Mtendaji Mkuu wa DSE Moremi Marwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao.


Na MWANDISHI WETU
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, amesema, uwekezaji mkubwa utakaofanywa na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania PLC baada ya kuorodheshwa rasmi katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) jana utasaidia kuongeza mapato ya Serikali na kuwezesha wananchi.
Kampuni hiyo jana ilijiorodhesha hisa zake DSE baada ya kuuza asilimia 25%  ya hisa zake ambapo kiasi cha shilingi bilini 476 kimefanikiwa kukusanywa.
Akizungumza wakati wa hafla fupi ya uorodheshaji wa hisa hizo, Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango,  alisema uoredheshwaji huo ni hatua muhimu ya kuwawezesha wananchi kiuchumi.
 “Mgawanyo wa hisa zilizouzwa kwa umma umefanyika kwa kutoa kipaumbele kwa wawekezaji wa ndani ya Tanzania ambapo wamepata aslimia 100% ya maombi yao ya waliofanya katika ununuzi wa hisa zilizouzwa kwa umma na hivyo hivyo wawekezaji wa ndani kupata asilimia 60% na wawekezaji wa kimataifa asilimia 40%,”.
Waziri Mpango alisema kipaumbele kimetolewa kwa wawekezaji wa ndani ili kuwezesha Watanzania kuwa washiriki katika maendeleo ya uchumi wa nchi yao badala ya kuachwa pembeni ya mageuzi na maendeleo ya kiuchumni yanayotokea hapa nchini.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao alimwambia Waziri Mpango kuwa fedha zilizokusanywa zitatumika kufanya uwekezaji zaidi na hivyo kuwafanya wawekezaji wapya kunufaika na uwekezaji wao ndani ya Vodacom Tanzania.
“Tutaendelea kufanya uwekezaji mkubwa na wenye tija kwa ajili ya wanahisa wetu. Vodacom ndiyo kampuni ya simu za mkononi inayoongoza na kupitia uwezeshaji huu wa kimtaji tunatarajia kukuwa zaidi,”alisema
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana Dk John Mduma alisema mafanikio hayo yanaleta chachu ya maendeleo na mageuzi katika sekta ya masoko ya mitaji na fedha hapa nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad