Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii.
Miss
Tanzania, Shose Sinare ameuomba upande wa mashitaka katika kesi ya
utakatishaji fedha inayomkabili, pamoja na wenzake wawili walete
mawasiliano yanayofanyika kati ya Tanzania na Uingereza juu ya
upelelezi dhidi ya kesi yao.
Shose
amedai hivyo leo katika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele
ya Hakimu Mkazi Cyprian Mkeha, Mbali na Sinare, washitakiwa wengine ni
katika kesi hiyo ni Kamishna Mkuu Mstaafu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA), Harry Msamire Kitilya, na Sioi Solomon.
Sinare
alidai kuwa mpaka sasa wamekaa gerezani kwa zaidi ya mwaka na nusu
hivyo upande wa mashitaka uwasilishe mawasiliano hayo.
Mapema,
Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi aliieleza mahakama
kuwa upelelezi bado haujakamilika kwani bado wanasubiri awamu ya pili ya
upelelezi huo.
Kufuatia
hayo, Hakimu Mkeha ameahirisha kesi hiyo hadi Agosti 25 mwaka huu ili
upande wa mashitaka ueleze muendelezo wa kile kilichowasilishwa kortini.
Katika kesi hiyo washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama,
kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha fedha.
Wanadaiwa
kutenda makosa hayo kati ya Machi 2013 na Septemba 2015 wakati wa
mchakato wa mkopo wa dola za Marekani milioni 550 kwa serikali ya
Tanzania kutoka Benki ya Standard Uingereza.
Katika
kesi hiyo, inadaiwa kuwa Agosti 2, 2012 Sinare kwenye Makao Makuu ya
benki ya Stanbic iliyopo Kinondoni kwa nia ya kudanganya aliandaa
nyaraka ya pendekezo akijaribu kuonyesha kuwa Benki ya Standard ya
nchini Uingireza ikishirikiana na benki ya Stabic ya Tanzania watatoa
mkopo wa dola za kimarekani milioni 550 kwa serikali ya Tanzania kwa
ada ya uwezeshaji ya asilimia 2.4 ya kiasi cha mkopo huo wakati akijua
kuwa sio kweli.
Inadaiwa
kuwa Agosti 2, 2012 ,Sinare alitoa nyaraka za uongo za mapendekezo ya
kuonyesha kuwa Benki ya Standard ya nchini Uingireza ikishirikiana na
benki ya Stabic ya Tanzania, watatoa mkopo wa dola za kimarekani
milioni 550 na kuziwasilisha katika ofisi za Wizara ya fedha wakati
akijua kuwa sio kweli.
Aliendelea
kudaiwa kuwa Septemba 20, 2012 katika Makao Makuu ya Benki ya Stanbic
nchini yaliyopo Kinondoni, alitenda kosa la kughushi barua.
Sinare
anadaiwa kughushi barua ya mapendekezo ikionyesha kuwa Benki ya
Standard ya nchini Uingireza ikishirikiana na benki ya Stabic ya
Tanzania watatoa mkopo wa dola za kimarekani milioni 550 kwa Serikali
ya Tanzania kama ada ya uwezeshaji wa asilimia 2.4 ya kiasi cha mkopo
huo wakati akijua kuwa sio kweli.
Agosti
21,2012, Sinare anadaiwa kuwa kwa lengo la kulaghai aliwasilisha
nyaraka hizo za uongo kuiwezesha Serikali ya Tanzania kupata mkopo huo
wa kiasi hicho cha ada ya uwezeshaji, katika ofisi za Wizara ya Fedha.
Washtakiwa
hao kwa pamoja wanadaiwa kughushi nyaraka za makubaliano kwamba
Novemba 5 ,2012 katika benki ya Stanbic makao makuu Kinondoni Dar es
Salaam, kwa nia ya kudanganya walighushi waraka wa makubaliano wa
Novemba 5, 2012.
Inadaiwa
kuwa waraka huo ulikusudia kuonesha kuwa Stanbic Tanzania imeingia
makubaliano ya ushirikiano na kampuni ya Enterpirise Growth Market
Advisors (Egma) Limited kuwezesha upatikanaji wa mkopo wa Dola za
Marekani milioni 550 kwa ajili Serikali ya Tanzania .
Wanadaiwa
kuwa Machi 2013 jijini Dar es Salaam walijipatia Dola za Marekani
milioni sita, wakionyesha kuwa fedha hizo zilikuwa ni malipo ya ada ya
uwezeshaji upatikanaji wa mkopo na zililipwa kupitia Kampuni ya Egma T
Ltd. Washtakiwa hao wanadaiwa kutakatisha fedha kwa kuhamisha,
kuchukua na kuweka kiasi cha Dola za Marekani milioni sita katika
akaunti tofauti tofauti za benki.
Kati
ya Machi 2013 na Septemba 2015, wanadaiwa kuwa waliweka pesa hizo
katika akaunti mbalimbali zilizomilikiwa na kampuni ya Egma na kwamba
walipaswa kufahamu kuwa pesa hizo ni mazao ya uhalifu wa kughushi.
No comments:
Post a Comment