Mshindi wa Tuzo ya International Confederation of Midwives (ICM), Loveluck Mwasha akiwasilisha mada kwenye kongamano la kuadhimisha Siku ya Wakunga Duniani lililofanyika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo. Maadhimisho hayo yalianza wiki iliyopita kwa kupima afya watu mbalimbali waliojitokeza katika hospitali hiyo. Siku ya Wakunga Duniani huadhimishwa Mei 5, kila mwaka, lakini TAMA tawi la Muhimbili iliamua kuadhimisha siku hii katika wiki ya unyonyeshaji duniani.
Baadhi ya Wakunga na maofisa wengine wakifuatilia kongamano hilo leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
No comments:
Post a Comment