Meya wa Wilaya ya Temeke, Abdallah Chaurembo akizungumza wakati wa
kikao cha baraza la madiwani wakati wa kufanya uchaguzi wa Naibu Meya ambapo kisheria kila mwaka hupatikana Naibu Meya mpya.
Halmashauri ya Manispaa ya Temeke imepata Naibu Meya mpya, katika kikao cha baraza la madiwani ambapo kisheria kila mwaka hupatikana Naibu Meya mpya.
Katika uchaguzi huo kulikua na wagombea wawili ambapo diwani wa kata ya Changombe
Benjamini Ndalichako akichuana na
diwani wa kata ya kurasini
Rajab Mkenga
.
Ambapo katika kinyangiro hicho Rajabu Mkenga aliibuka mshindi kwa kura 18 kati ya kura 29 kati ya kura zilizopigwa,huku mpinzani wake akiwa na kura 11.
Mara baada ya kupata ushindi huo Mkenga aliwashukuru wapiga kura wote na kuwaomba washirikiane katika kuijenga Temeke mpya.
Pia katika baraza hilo ulifanyika uchaguzi wa viongozi wa kamati mbalimbali ambazo zitashirikiana katika mambo ya kijamii na maendeleo ya Temeke, kamati hizo ni pamoja na kamati ya uchumi na uongozi, kamati ya mipango miji, kamati ya Afya Elimu na Uchumi,Kamati ya nidhamu na maadili, Kamati ya Fedha na uongozi na kamati ya kugawa Ardhi.
Madiwani wakiwa wanafuatilia
kikao cha baraza la madiwani wakati wa kufanya uchaguzi wa Naibu Meya ambapo kisheria kila mwaka hupatikana Naibu Meya mpya.
No comments:
Post a Comment