HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, August 25, 2017

ATE YAZINDUA TUZO ZA KUMPATA MWAJIRI BORA KWA MWAKA WA 2017

 Mkurugenzi Mtendaji wa ATE  Dkt Aggrey Mlimuka  akielezea maboresho mbalimbali waliyoyafanya katika nyanja za kumpata Mwajiri bora wa mwaka 2017 na kuzindua rasmi kuanza kumsaka mshindi wa mwaka huu kutoka kwa washiriki wanachama 1400 wa ATE, Kushoto ni Mratibu wa tuzo za Mwajiri bora Joyce Nangai na Mkurugenzi usimamizi wa fedha na utawala Dr Amrose Kessy.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

CHAMA cha Waajiri Nchini (ATE)  kimezindua rasmi Tuzo ya Mwajiri Bora kwa mwaka 2017 ikiwa ni katika kulenga tathmini mchango wa rasilimali watu ili kuwawezesha kushiriki katika utendaji wa masuala mbalimbali ya kibishara.

ATE ina jumla hya wanachama washiriki 1400 kutoka sekta binafsi na wengine 6000 wasio wanachama wa moja kwa moja wanaotoka makampuni ya biashara na baadhi ya mashirika ya umma.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa tuoz hizo zilizoanza mwaka 2005 zikijulikana kam EYA, Mkurugenzi Mtendaji wa ATE  Dkt Aggrey Mlimuka amesema kwamba tuzo ya mwajiri bora wa mwaka inalenga zaidi katika kuwatambua wanachama wake waliofanya vizuri katika kuweka mikakati bora ya kutathimini usimamizi wa rasilimali watu na shughuli za kibiashara.

Dkt Mlimuka amesema kuwa tuzo hizi zimehamasisha makampuni wanachama kuweka juhudi katika masuala ya ajira na usimamizi wa rasilimali watu kama msingi wa mikakati ya makampuni yao kujenga  nguvu kazi yenye ujuzi, furaha, ushindani na yenye kushiriki kikamilifu katika uzalilishaji.
Mkurugenzi Mtendaji wa TanzConsult Prof Beatus Alois Thomas akizungumzia namna watakavyotumia dodoso mbalimbali zitakazotumika kumpata Mwajiri bora kwa mwaka 2017 ikiwa ni mara ya pili kuweza kusimamia toka kuzishwa kwa tuzo hizo nchini.

Tuzo za mwaka huu zimeweza kuboreshwa katika mahitaji hasa ya kibiashara na naadhi ya vigezo vimeboreshwa  na zikijikita hasa kataika nyanja za Afya, uwiano wa kazi na maisha, waajii wanaochochea na kuwajali wafanyakazi wake, mahusiano mazuri baina ya waajiri na waajiriwa, kuwekeza katika teknolojia pamoja nadhana ya utofautishwaji na ushirikishwaji.

Upatakinaji wa mshindi wa tuzo wa mwajiri bora wa mwaka utasimamiwa na TanzConsult chini ya Prof Beatus Alois Thomas na usimamizi wa pili wa matukio mpaka kilele cha sherehe ambapo zinatarajiwa kufanyika Desemba 08 mwaka huu wakitarajiwa mgeni rasmi kuwa mmoja wa viongozi wakuu wa kitaifa.

Dkt Mlimuka aliweza kusema kuwa kwa mwaka watakuw ana tuzo za aina mbili, moja ikiwa ni kwa ajili ya makampuni binafsi na nyingine ni kwa mashirika ya serikali ili kutoa fursa na kwa upande wao kuweza kushiriki katika tuzo hizo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad