HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, July 13, 2017

UZINDUZI REA AWAMU YA TATU MWANZA, WAFANA

 Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani akielezea mikakati ya serikali ya kupeleka umeme katika vijiji na vitongoji vyote mkoani Mwanza kupitia  Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu kwenye uzinduzi huo.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akielezea hali ya umeme katika mkoa huo kwenye uzinduzi huo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini, Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga (kushoto)  na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini Dkt. Gideon Kaunda  (kulia) wakifuatilia  hotuba iliyokuwa inatolewa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani ( hayupo pichani) kwenye uzinduzi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu kwa mkoa wa Mwanza uliofanyika katika kijiji cha Nyamatala wilayani Kwimba mkoani humo tarehe 13 Julai, 2017.
 Sehemu ya  wananchi wa kijiji cha Nyamatala wilayani Kwimba mkoani Mwanza wakifuatilia hotuba ya uzinduzi iliyokuwa inatolewa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani ( hayupo pichani) kwenye uzinduzi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu kwa mkoa wa Mwanza uliofanyika katika kijiji cha Nyamatala wilayani Kwimba mkoani humo tarehe 13 Julai, 2017.
 Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa akieleza jambo kwenye uzinduzi huo.
 Sehemu ya wataalam kutoka mkandarasi atakayejenga miundombinu ya umeme katika mkoa wa Mwanza kupitia Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu wakisikiliza maelekezo kutoka kwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani (hayupo pichani) kwenye uzinduzi huo.
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani (katikati) akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu kwa mkoa wa Mwanza.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani (wa tano kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella (wa sita kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na wabunge, watendaji kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Shirika la  Umeme  Tanzania (TANESCO) na viongozi wengine wa kitaifa mara baada ya kumalizika kwa uzinduzi huo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad