HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, July 11, 2017

Ujumbe wa Tanzania washiriki Mkutano wa 36 wa SADC

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo, Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Emmanuel Kolobelo unashiriki  Mkutano wa 36 wa Mawaziri wa Nishati na Maji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), nchini Swaziland.
Mkutano huo uliofunguliwa na Waziri Mkuu wa Swaziland, Dkt. Sibusiso Dlamin umehudhuriwa na nchi mbalimbali ikiwemo  Tanzania, Malawi, Zambia, Zimbabwe, Lesotho, Swaziland, Botswana, Msumbiji, Namibia, Seychelles, Botswana, Madagascar na Mauritius.
Mkutano huo umeanza tarehe 8 Julai, 2017 na utamalizika tarehe 11 Julai, 2017.
 Waziri Mkuu wa Swaziland, Dkt. Sibusiso Dlamin akifungua Mkutano wa 36 wa Mawaziri wa Nishati na Maji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) unaofanyika nchini Swaziland.
Ujumbe wa Tanzania unaoshiriki  mkutano wa 36 wa Mawaziri wa Nishati na Maji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), nchini Swaziland, kutoka kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo, Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Emmanuel Kolobelo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad